Biblia—Kiongozi Ambacho Mungu Amewapa Watu Wote
1 Biblia zinazokadiriwa kuwa bilioni nne zimechapwa katika lugha na lahaja zaidi ya 2,100, zikifanya Neno la Mungu lipatikane kwa zaidi ya asilimia 90 ya idadi ya watu wa dunia. Na bado, kuna njaa ulimwenguni ya “kuyasikia maneno ya BWANA.” (Amo. 8:11) Watu wengi walio na nakala ya Biblia ama hawaisomi ama hawaelewi yaliyomo. Twaweza kuwachocheaje watumie Biblia kuwa kiongozi chenye kutumika katika maisha yao?
2 Tutatoa kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? pamoja na Biblia Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo mwezi wa Desemba. Hilo laweza kufanywa kwa kutoa kielezi cha usemi wake ulio wazi, na wa kisasa. (Ona kitabu “Kila Andiko,” ukurasa wa 328, fungu la 6.) Tutaonyesha uthamini wetu mkubwa kwa zawadi hii kutoka kwa Yehova kwa kusaidia wengine kwa idili waikubali Biblia kuwa kiongozi ambacho Mungu amewapa watu wote.
3 Ungeweza kutoa utangulizi wa utoaji kwa kutumia trakti “Sababu Kwa Nini Wewe Unaweza Kuitumaini Biblia.” Waweza kusema hivi:
◼ “Hata ingawa Biblia yapatikana kwa zaidi ya asilimia 90 ya idadi ya watu wa ulimwengu, watu wachache huisoma kwa ukawaida. Unafikiri sababu ni nini?” Soma mafungu ya kwanza mawili ya trakti hiyo, pamoja na 2 Timotheo 3:16. Toa kitabu Neno la Mungu pamoja na Tafsiri ya Ulimwengu Mpya kwa mchango wake wa kawaida. Kitabu kisipochukuliwa, mwombe mwenye nyumba asome sehemu inayobaki ya trakti kwa wasaa wake. Kazia kichwa kidogo cha mwisho, “Kuutabiri Wakati Ujao.”
4 Unaporudia watu ambao uliachia trakti “Sababu Kwa Nini Wewe Unaweza Kuitumaini Biblia,” waweza kujaribu huu:
◼ Baada ya kujijulisha, soma mafungu mawili ya mwisho ya trakti hiyo. Mwulize mwenye nyumba kama alipata wakati kufikiria uwezekano wowote wa kuishi milele duniani. Baada ya kuitikia, sema: “Mashahidi wa Yehova wana hakika ya kwamba unabii wote unaopatikana katika Biblia utatimizwa, kutia na ule unaotabiri wakati ujao ulio mzuri ajabu kwa watu wote wanaotimiza matakwa ya Mungu.” Onyesha picha iliyo kwenye ukurasa wa 13 katika broshua Anataka, rudi nyuma kwenye somo la 5, na ujitolee kuzungumzia majibu ya maswali yaliyoorodheshwa, hivyo ukianzisha funzo.
5 Katika eneo ambalo watu ni wa kidini, waweza kujaribu mfikio huu wa kwanza:
◼ “Twatia moyo watu wastahi zaidi Biblia. Familia nyingi zina Biblia, lakini ni mara chache tu wanapoirejezea wanapokuwa na matatizo mazito. Je, wewe umeona hilo? [Ruhusu itikio.] Labda wanaamini kwamba Biblia ni ya zamani. Kitabu hiki, Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, hutoa uthibitisho wenye kusadikisha kwamba Biblia ni sahihi kisayansi na kwamba huandaa matatuzi yenye kutumika kwa matatizo ya leo yenye kusonga.” Kazia mambo makuu machache kutoka sura ya 8 au sura ya 12 ya kitabu hicho, kisha ukitoe.
6 Unapofuatia angusho la kitabu “Neno la Mungu,” ungeweza kusema:
◼ “Nilipokutembelea mara ya mwisho, tulizungumza jinsi ambavyo Biblia husaidia kutatua matatizo magumu ya leo. Wale ambao wameikubali kuwa Neno la Mungu pia wamesaidiwa kuishi maisha yenye furaha, yenye uradhi. Ningependa kukuonyesha mojawapo ya kanuni za Biblia yenye kutumika inayoelezwa katika kitabu nilichokuachia.” Zungumzia mojawapo ya kanuni za Kimaandiko zipatikanazo katika sura ya 12, fungu la 3-6, na umalizie kwa kusoma fungu la 7. Kupendezwa kukionyeshwa, toa funzo katika ama kitabu Ujuzi au broshua Anataka.
7 Utoaji ufuatao huenda ukapendeza watu wenye umri mkubwa zaidi:
◼ “Kulikuwa na wakati ambao Biblia ilisomwa katika nyumba zilizo nyingi na wakati familia zilipoishi kulingana na kanuni zake. Je, ilikuwa hivyo katika familia yako? [Ruhusu itikio.] Leo yaonekana kwamba wengi wanakengeushwa kutumia wakati wao ili kusoma Biblia au wanahisi kwamba kanuni zake za adili ni za zamani. Sura ya 13 ya kitabu hiki, Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, hutoa mambo yaliyoonwa matatu ya kweli ya watu ambao maisha yao yalibadilika yakawa bora baada ya kujifunza Biblia. Ikiwa ungependa kusoma jinsi nguvu ya Neno la Mungu ilivyowasaidia, nitafurahi kukuachia kitabu hiki.”
8 Kwenye ziara ya kurudia, ungeweza kusema hivi:
◼ “Tulipoongea mara ya mwisho, tulikubaliana kwamba kanuni za Biblia za adili zinapuuzwa katika jamii ya leo. Je, ukosefu huo wa staha utuhangaishe? [Ruhusu itikio.] Yesu Kristo alithamini sana kutwaa ujuzi wa Biblia.” Soma Yohana 17:3. Kisha shiriki fungu la 5 la sura ya 1 katika kitabu Ujuzi. Eleza juu ya programu yetu ya funzo la Biblia bila malipo, na ujitolee kulionyesha.
9 Sali kwamba Yehova abariki jitihada zako za kuelekeza fikira kwenye Biblia—kiongozi ambacho Mungu amewapa watu wote.