Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/98 kur. 3-6
  • Je, Tutaufanya Tena?—Mwito Mwingine wa Mapainia-Wasaidizi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Tutaufanya Tena?—Mwito Mwingine wa Mapainia-Wasaidizi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari Zinazolingana
  • Wanatakwa—Mapainia-Wasaidizi 2,500
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Mradi Mzuri kwa Ajili ya Mwaka Mpya wa Utumishi
    Huduma ya Ufalme—2007
  • Tangazeni Kotekote Sifa Bora za Yehova
    Huduma ya Ufalme—2007
  • Majira ya Ukumbusho Ni Wakati wa Kuongeza Utumishi
    Huduma ya Ufalme—2005
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 3/98 kur. 3-6

Je, Tutaufanya Tena?—Mwito Mwingine wa Mapainia-Wasaidizi

1 Ni nini tutakachofanya tena? Je, tutafanya upainia-msaidizi majira ya Ukumbusho? Nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Februari 1997 ilinasa uangalifu wetu kwenye kichwa hiki chenye maandishi mazito: “Wanatakwa—Mapainia-Wasaidizi 2,500.” Tulikuwa na uhakika mngechukua mwito huo kwa uzito. Ripoti ya utumishi ya Machi 1997 ilipokusanywa tulipendezwa kujua kwamba watu 3,497 walikuwa wamejiandikisha kuwa katika utumishi wa painia-msaidizi! Tukiongezea idadi hiyo mapainia wa kawaida 2,645 na mapainia wa pekee 449 walioripoti mwezi huo, twaona kwamba karibu asilimia 26 ya wahubiri ilikuwa katika utumishi wa painia. Je, tutaufanya tena majira haya ya Ukumbusho?

2 Twawapongeza kwa uchangamfu, wote waliotia jitihada ya ziada kuongeza utendaji wao wa shambani miezi ya mwaka uliopita ya Machi, Aprili, na Mei. Kwa wazi, nyinyi nyote mlichochewa na upendo wenu usio na ubinafsi kwa Yehova Mungu na kwa jirani yenu. (Luka 10:27; 2 Pet. 1:5-8) Wahubiri waliokuwa katika hali mbalimbali za maisha walifanya mipango ya kushiriki katika upainia-msaidizi. Katika kutaniko moja, wahubiri 51 walipainia pamoja mwezi huohuo, kutia ndani wazee walio wengi, mama mwenye binti wa umri wa miezi 15, dada aliyeacha kazi yake na kupata kazi isiyo ya wakati wote ili kumwezesha kupainia, na dada mmoja mwenye umri mkubwa zaidi ambaye hakupata kamwe kupainia kabla ya hapo. Mwangalizi wa mzunguko aliandika hivi: “Jitihada kubwa zaidi katika kazi ya kuhubiri yaendelea. . . . Hilo haliwi na matokeo tu kwenye eneo bali makutaniko yanabubujika kwa uchangamfu. Akina ndugu wanafurahia kupata kujuana vizuri zaidi na vilevile kuona matokeo mazuri katika huduma.”

3 Vijana walitiwa ndani pia. Mhubiri asiyebatizwa mwenye umri wa miaka 13 alikuwa akitazamia wakati ambapo angefananisha wakfu wake kwa Yehova. Baada ya kubatizwa Februari, aliandika kuhusu tamaa yake ya kufanya upainia-msaidizi katika Machi: “Sasa nikiwa sina kitu cha kunizuia, nilijaza ombi langu mara moja. . . . Mambo mengi mazuri ajabu tuliyofurahia hayangalitokea kama haingalikuwa kwa sababu ya mwaliko wenu wenye upendo wa kutualika tupainie. Namshukuru Yehova kwa vile nilikuwa nimepata pendeleo hili kuwa miongoni mwa wale [2,500] walioitikia.” Yeye ameweka mradi wa kuufanya tena.

4 Labda ulikuwa miongoni mwa wale 3,497 walioshiriki katika utendaji wa painia-msaidizi mwezi wa Machi uliopita, au 3,213 katika Aprili, au wale 2,279 katika Mei. Je, utaufanya tena mwaka huu? Ikiwa hukuweza kufanya upainia miezi ya mwaka uliopita ya Machi, Aprili, na Mei, je, waweza kuufanya mwaka huu? Je, twaweza kupita 3,497, ile idadi ya waliofanya upainia-msaidizi katika Machi 1997? Hiyo ilikuwa idadi kubwa zaidi ya mapainia-wasaidizi katika mwezi wowote ule katika nchi zote zilizo chini ya ofisi ya tawi yetu.

5 Makinikia Aprili na Mei: Mwaka huu, Ukumbusho utakuwako Jumamosi, Aprili 11, ukifanya Aprili kuwa mwezi bora kabisa kwa ajili ya utendaji ulioongezeka katika huduma. (2 Kor. 5:14, 15) Wakati wa siku 11 za kwanza za mwezi, tutakazia uangalifu kualika watu wenye kupendezwa wengi iwezekanavyo wahudhurie Ukumbusho. Ukipanga kufanya upainia-msaidizi, tafadhali toa ombi lako mapema kabla ya tarehe unayotaka kuanza.—1 Kor. 14:40.

6 Kwa kuwa mwezi wa Mei una miisho-juma mitano kamili, wahubiri walio shuleni au wanaofanya kazi ya kimwili wakati wote huenda wakaona kuwa rahisi kufanya upainia-msaidizi mwezi huo. Kwa kuratibu muda wa saa kumi katika utumishi wa shambani kila ya hiyo miisho-juma mitano, utahitaji kuratibu muda wa saa kumi tu za ziada mwezi huo ili kufikia kiwango cha saa 60 zinazotakwa.

7 Wakati wa Aprili na Mei, tutakuwa tukitoa maandikisho ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yakiwa toleo la fasihi. Hili lapaswa kutia moyo hata wengi wetu zaidi kufikia upainia. Kwa nini twasema hivyo? Ni rahisi kutoa magazeti nayo yanafurahisha kuyatumia katika huduma. Hayo yanaweza kutumiwa kwa kufaa katika sehemu zote za utumishi—nyumba hadi nyumba na duka hadi duka, na vilevile tunapofikia watu barabarani, maegeshoni ya magari, na katika bustani na vikao vinginevyo vya kivivi-hivi. La maana zaidi, Mnara wa Mlinzi na Amkeni! hutetea kweli za Ufalme. Hayo hukazia uangalifu utimizo wa unabii wa Biblia, yakithibitisha kwamba Ufalme wa Mungu unatawala. Pia huathiri maisha ya wasomaji kwa kushughulikia kwa uelewevu mahitaji halisi ya watu. Tufikiripo jinsi ambavyo maisha yetu yameathiriwa na majarida haya yenye thamani, tutachochewa kuyashiriki na kuyagawanya kwa wingi iwezekanavyo katika Aprili na Mei.

8 Katika kujitayarisha kwa ajili ya utendaji huu wa juhudi nyingi wa magazeti, utanufaika na kuzipitia makala hizi: “Mnara wa Mlinzi na Amkeni!—Majarida ya Wakati Ufaao Yenye Kweli” (Mnara wa Mlinzi, Januari 1, 1994), “Tumieni Magazeti Yetu Vema Kabisa” (Huduma ya Ufalme Yetu ya Septemba 1995), na “Tayarisha Utoaji Wako Mwenyewe wa Magazeti” (Huduma ya Ufalme Yetu ya Oktoba 1996).

9 Wazee Ongozeni: Ili kuwasaidia wahubiri wengi waliokuwa wakipainia miezi ya mwaka uliopita ya Machi, Aprili, na Mei, wazee katika kutaniko moja walitoa Jumamosi moja ya mwezi kuwa siku ya pekee ya utendaji wa utumishi wa kutaniko zima. Mipango ilifanywa ya kukutana mara kadhaa mbalimbali wakati wa siku hiyo, ikiwapa wote kutanikoni fursa ya kushiriki katika aina mbalimbali za kutoa ushahidi. Ilitia ndani kuhubiri kwenye sehemu za biashara, kutoa ushahidi barabarani, nyumba hadi nyumba, kufanya ziara za kurudia, kuandika barua, na kutoa ushahidi kupitia simu. Itikio lilikuwa lenye kutokeza, wahubiri 117 wakishiriki katika utumishi wa shambani katika muda wa siku hiyo. Walifanya jumla ya saa 521 zilizotumiwa katika huduma na maangusho 617 ya magazeti, broshua, na vitabu! Msisimko wa Jumamosi hiyo uliendelea hadi Jumapili, kukiwa na hudhurio kubwa zaidi kwenye Mkutano wa Watu Wote na Funzo la Mnara wa Mlinzi.

10 Katika kila Mkutano wa Utumishi Aprili na Mei, kutaniko lapasa kukumbushwa mahali na wakati mikutano ya utumishi wa shambani itakapofanywa juma litakalofuata, hasa ikiwa mipango ya ziada yafanywa tofauti na ile ambayo huratibiwa kwa kawaida. Mapainia wa kawaida na vilevile wahubiri ambao si mapainia-wasaidizi wanatiwa moyo kuunga mkono mipango ya kikundi kadiri hali zao ziruhusuvyo.

11 Mwangalizi wa utumishi atahitaji kukutana na ndugu ambaye hugawa maeneo ili kufanya mipango ya kuhubiri yale ambayo hayafanywi mara nyingi. Uangalifu mwingi waweza kukaziwa wasiokuwako nyumbani na kutoa ushahidi barabarani na duka hadi duka. Kutoa ushahidi jioni kwaweza kukaziwa, hasa mahali ambapo ziara za kurudia na mafunzo yanaweza kuongozwa jioni. Magazeti ya kutosha yapasa kuagizwa kwa ajili ya Aprili na Mei kwa kutazamia utendaji ulioongezeka.

12 Wahubiri Wengi Wanaweza Kuwa na Sifa ya Ustahili: Sentensi ya kwanza ya ombi la painia-msaidizi husema: “Kwa sababu nampenda Yehova na nataka sana kusaidia wengine wamjue yeye na makusudi yake yenye upendo, ningependa kuongeza ushiriki wangu katika utumishi wa shambani kwa kujiandikisha niwe painia-msaidizi.” Kumpenda Yehova na kutaka kusaidia wengine kiroho ndiyo mambo ya msingi ya wakfu wetu. (1 Tim. 4:8, 10) Ili mtu awe na sifa ya ustahili ya upainia-msaidizi, lazima abatizwe, awe na msimamo mzuri wa adili, na awe katika hali ya kutoa muda wa saa 60 kwenye huduma wakati wa mwezi. Sisi sote tufikiriapo hali zetu, je, baadhi yetu ambao hawajapata kupainia kamwe wanaweza kufanya hivyo mwaka huu Aprili au Mei?

13 Wengi katika makutaniko huenda wakatambua kwamba wangeweza kupainia wanapoona wengine wakijiandikisha ambao wana hali kama zao. Wanashule, wazee-wazee, kutia na wazee na watumishi wa huduma, na wengineo wamefanya upainia-msaidizi kwa mafanikio. Mke nyumbani mmoja aliye mama wa watoto wawili aliye na kazi ya wakati wote alifikisha saa 60, akaangusha magazeti 108, na kuanzisha mafunzo ya Biblia 3 katika mwezi mmoja wa kufanya upainia-msaidizi. Alifanyaje hivyo? Alitumia saa zake za chakula cha mchana kazini kutoa ushahidi katika eneo la karibu, alitoa ushahidi kupitia kuandika barua, na alishiriki katika kutoa ushahidi kwenye maegesho ya magari na barabarani. Pia alitumia siku yake ya mapumziko kila juma kwa manufaa kwa kushiriki katika utumishi wa shambani pamoja na kutaniko. Ijapokuwa hapo kwanza alifikiri kwamba upainia-msaidizi ulikuwa mradi usioweza kufikiwa, kwa kitia-moyo kutoka kwa wazee na ratiba itumikayo, vizuizi vilishindwa.

14 Yesu aliwahakikishia wanafunzi wake hivi: “Nira yangu ni ya fadhili na mzigo wangu ni mwepesi.” (Mt. 11:30) Hicho kilikuwa kichwa chenye kutia moyo cha makala moja katika Mnara wa Mlinzi, Agosti 15, 1995. Yazungumza kuhusu dada mmoja aliyekuwa na kazi ya kimwili yenye kutokeza mkazo mwingi sana, ya wakati wote. Je, alifikiri kufanya upainia-msaidizi kulikuwa kusikowezekana kwake? La. Kwa hakika, aliweza kufanya upainia-msaidizi kila mwezi. Kwa nini? Kwa sababu alihisi kwamba kupainia kwa kweli kulimsaidia aendeleze usawaziko wake. Kusaidia watu walipokuwa wakijifunza kweli ya Biblia na kuwaona wakibadili maisha zao ili kupata kibali cha Mungu kulikuwa chanzo cha shangwe katika maisha yake yenye shughuli nyingi.—Mit. 10:22.

15 Dhabihu na marekebisho yoyote mtu ahitajiyo kufanya ili kupainia huthawabishwa kwa wingi na baraka zifurahiwazo. Dada mmoja aliandika kuhusu jambo aliloona akifanya upainia-msaidizi: “Ulinisaidia kutojifikiria sana na kukazia fikira zaidi kuwasaidia wengine. . . . Naupendekeza kwa wale wawezao kuufanya.”

16 Hutaka Ratiba Nzuri: Kwenye ukurasa wa mwisho wa nyongeza hii, tumetokeza tena ratiba za mfano zilizokuwa katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Februari 1997. Labda mojapo ya hizi yafaa hali zako. Unapozipitia, fikiria kwa uangalifu kawaida yako ya kila siku ya utendaji wa kila mwezi. Ni mambo gani nyumbani mwako yanayoweza kufanywa kabla ya kupainia kwako au yanayoweza kuwekwa kando hadi baadaye? Je, baadhi ya wakati unaotumia katika vitumbuizo, tafrija, au aina nyingine za wasaa wa mapumziko zaweza kuondoshwa? Badala ya kutazama jumla ya saa 60 zinazohitajiwa, panga ratiba yako kwa msingi wa kila siku au wa kila juma. Ni saa 2 tu kwa siku au 15 kwa juma zinazohitajiwa ili kufanya upainia-msaidizi. Tazama ratiba za mfano, na ukiwa na penseli, ona kile unachoweza kukadiria kuhusu ratiba ya utumishi ya kibinafsi inayokufaa vizuri wewe na familia yako.

17 Itikio zuri na tegemezo ambalo kutaniko lilionyesha kwa ajili ya huduma miezi ya mwaka uliopita ya Machi, Aprili, na Mei lilichochea shauku ya painia wa kawaida mmoja ambaye aliandika hivi: “Asanteni sana kwa kitia-moyo chenu chenye upendo cha kutia jitihada ya ziada ya kutegemeza upainia-msaidizi. . . . Ratiba zenu zilizodokezwa zilisaidia wengine ambao hawakuwa wamepata kupainia, kuona kwamba wangeweza kuufanya. . . . Nina furaha sana kuwa sehemu ya tengenezo la Yehova na kufuata uongozi wake wenye upendo wa mtumwa mwaminifu na mwenye busara.”

18 Mithali 21:5 (NW) hutuhakikishia hivi: “Mipango ya mwenye bidii bila shaka huleta manufaa.” Mithali 16:3 hututia moyo hivi: “Mkabidhi BWANA kazi zako, na mawazo [“mipango,” NW] yako yatathibitika.” Naam, kwa kumtia Yehova katika uamuzi wetu kwa njia ya sala na kumtegemea imara atusaidie tufaulu, twaweza kuwa na mtazamo chanya kuhusu mipango yetu ya upainia-msaidizi. Huenda ikawa kwamba baada ya kuona vizuri jinsi ratiba yetu inavyofanya kazi kwa mwezi mmoja au miwili ya kufanya upainia-msaidizi, tutaweza kulitia alama sanduku lililo kwenye ombi la painia-msaidizi ambalo husomeka hivi: “Tia alama hapa ikiwa unataka kutumikia ukiwa painia-msaidizi mfululizo mpaka taarifa ya kuacha itakapotolewa.” Kwa vyovyote, twaweza kutazamia kufanya upainia-msaidizi tena katika Agosti, ambapo kutakuwa na miisho-juma mitano kamili. Tumaliziapo mwaka wa utumishi katika Agosti, jitihada ya pamoja itafanywa ili kila mtu ashiriki katika huduma kikamili iwezekanavyo.

19 Yesu alitabiri hivi: “Yeye ambaye hudhihirisha imani katika mimi, huyo pia atafanya kazi ambazo mimi hufanya; naye atafanya kazi kubwa zaidi ya hizi.” (Yn. 14:12) Ni pendeleo letu lenye shangwe kutumika tukiwa wafanyakazi wenzi wa Mungu wakati unabii huu unapokuwa na utimizo mkuu. Sasa ndio wakati wa kuhubiri habari njema kwa juhudi nyingi kuliko wakati wowote ule, tukinunua wakati unaofaa wa kufanya kazi hii. (1 Kor. 3:9; Kol. 4:5) Kushiriki mara nyingi iwezekanavyo katika utumishi wa painia-msaidizi ni njia bora kabisa ya kufanya sehemu yetu tukiwa wapiga-mbiu wa Ufalme. Twangoja kwa hamu kuona jinsi wimbo wa sifa utakavyokuwa mkubwa majira haya ya Ukumbusho kutoka kwa mapainia-wasaidizi. (Zab. 27:6) Tukifikiria matokeo ya miezi ya mwaka uliopita ya Machi, Aprili, na Mei, twajiuliza, ‘Je, tutaufanya tena?’ Tuna hakika kwamba tutaufanya!

[Sanduku katika ukurasa wa 3]

Je, Waweza Kufanya Upainia-Msaidizi?

“Hata uwe una hali gani za kibinafsi, kama umebatizwa, una hali nzuri ya kiadili, unaweza kufanya mpango utimize takwa la kutumia kila mwezi saa 60 katika huduma ya shambani na unaamini ungeweza kutumika kuwa painia-msaidizi mwezi mmoja au zaidi, wazee wa [kutaniko] watafurahi kufikiria ombi lako la pendeleo hili la utumishi.”—Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu, ukurasa wa 113-114.

[Sanduku katika ukurasa wa 6]

Ratiba za Painia-Msaidizi

Njia za Mfano za Kuratibu Saa 15 za Utumishi wa Shambani Kila Juma

Asubuhi—Jumatatu hadi Jumamosi

Jumapili yaweza kubadilishwa na siku yoyote

Siku Kipindi Saa

Jumatatu Asubuhi 2 1⁄2

Jumanne Asubuhi 2 1⁄2

Jumatano Asubuhi 2 1⁄2

Alhamisi Asubuhi 2 1⁄2

Ijumaa Asubuhi 2 1⁄2

Jumamosi Asubuhi 2 1⁄2

Jumla ya Saa: 15

Siku Mbili Kamili

Siku zozote mbili za juma zaweza kuchaguliwa

Siku Kipindi Saa

Jumatano Siku Nzima 7 1⁄2

Jumamosi Siku Nzima 7 1⁄2

Jumla ya Saa: 15

Jioni Mbili na Mwisho-Juma

Jioni mbili zozote za katikati ya juma zaweza kuchaguliwa

Siku Kipindi Saa

Jumatatu Jioni 1 1⁄2

Jumatano Jioni 1 1⁄2

Jumamosi Siku Nzima 8

Jumapili Nusu Siku 4

Jumla ya Saa: 15

Alasiri za Katikati ya Juma na Jumamosi

Jumapili yaweza kubadilishwa na siku yoyote

Siku Kipindi Saa

Jumatatu Alasiri 2

Jumanne Alasiri 2

Jumatano Alasiri 2

Alhamisi Alasiri 2

Ijumaa Alasiri 2

Jumamosi Siku Nzima 5

Jumla ya Saa: 15

Ratiba Yangu Binafsi ya Utumishi

Amua juu ya kiasi cha saa za kila kipindi

Siku Kipindi Saa

Jumatatu

Jumanne

Jumatano

Alhamisi

Ijumaa

Jumamosi

Jumapili

Jumla ya Saa: 15

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki