Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/00 uku. 8
  • Msongo wa Marika na Pendeleo Lako la Kuhubiri

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Msongo wa Marika na Pendeleo Lako la Kuhubiri
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Vijana Wenzako Wanaweza Kukuathiri Sana?
    Amkeni!—2002
  • Jinsi ya Kuepuka Kushinikizwa na Marafiki
    Amkeni!—2014
  • Nawezaje Kuepuka Kuathiriwa na Vijana Wenzangu?
    Amkeni!—2002
  • Vijana—Msikubali Kusongwa na Marafiki
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 12/00 uku. 8

Msongo wa Marika na Pendeleo Lako la Kuhubiri

1 Msongo wa marika ni uvutano wenye nguvu sana—kwa uzuri au kwa ubaya. Watumishi wa Yehova wenzetu huwa na uvutano mzuri unaotuchochea kufanya kazi zilizo bora za Kikristo. (Ebr. 10:24) Hata hivyo, washiriki wa familia wasio Mashahidi, wafanyakazi wenzetu, wanashule wenzetu, majirani, au watu wengine tunaofahamiana nao wanaweza kutusonga tufuate mwendo usiopatana na kanuni za Kikristo. Huenda wakasema “kwa kushushia heshima mwenendo [wetu] mwema kuhusiana na Kristo.” (1 Pet. 3:16) Twaweza kudumishaje azimio letu la kuendelea kuhubiri ujapokuwa msongo usiofaa wa marika ambao huenda tukakabili?

2 Washiriki wa Familia: Nyakati nyingine, mume na baba ambaye si mmoja wa Mashahidi wa Yehova huenda asitake mke wake na watoto wake washiriki katika huduma ya peupe. Ndivyo ilivyokuwa kwa familia moja huko Mexico. Mke na watoto saba wa mwanamume mmoja waliingia katika kweli. Mwanzoni aliwapinga kwa sababu hakutaka familia yake ihubiri na kutoa vichapo vya Biblia nyumba hadi nyumba. Alihisi kwamba hilo liliwashushia heshima. Hata hivyo, mke wake na watoto wake walishikilia imara uamuzi wao wa kumtumikia Yehova na kushiriki kwa ukawaida katika huduma. Baada ya muda, mwanamume huyo alianza kuona thamani ya kukubali mpango wa Mungu wa kazi ya kuhubiri, naye pia akajiweka wakfu kwa Yehova. Ilimchukua miaka 15 kukubali kweli, lakini je, angefanya hivyo kama familia yake haingeendelea na pendeleo lao la kuhubiri?—Luka 1:74; 1 Kor. 7:16.

3 Wafanyakazi Wenzako: Huenda jitihada zako za kuhubiria wafanyakazi wenzako zisikubaliwe na wengine. Dada mmoja alisimulia kwamba walipokuwa na mazungumzo juu ya mwisho wa ulimwengu ofisini, alidhihakiwa kwa sababu alidokeza wasome Mathayo sura ya 24. Hata hivyo, siku chache baadaye, mmoja wa wafanyakazi wenzake alimwambia kwamba alisoma sura hiyo na akaifurahia sana. Alimwachia kichapo, na mipango ikafanywa ya kumfunza Biblia pamoja na mume wake. Funzo la kwanza liliendelea hadi saa nane za usiku. Baada ya kujifunza mara tatu, walianza kuhudhuria mikutano, na punde baada ya hapo wakaacha kutumia tumbaku na kuanza kushiriki katika huduma. Je, jambo hilo lingetokea ikiwa dada yetu hangejitahidi kushiriki tumaini lake na wengine?

4 Wanashule Wenzako: Ni jambo la kawaida kwa vijana Mashahidi kupatwa na msongo wa marika shuleni na kuogopa kwamba vijana wengine watawadharau kwa sababu ya kuhubiri. Kijana mmoja Mkristo huko Marekani alisema: “Nilikuwa na woga wa kuhubiria vijana wengine kwa sababu niliogopa kutaniwa.” Kwa hiyo aliepuka fursa za kuhubiria marika wake shuleni na katika eneo. Waweza kusitawishaje nguvu ya kuwa na ujasiri kuelekea msongo wa marika? Mtumaini Yehova, ukitafuta kibali chake. (Mit. 29:25) Onea fahari uwezo wako wa kutumia Neno la Mungu katika huduma yako. (2 Tim. 2:15) Kijana aliyenukuliwa hapo juu alianza kusali kwa Yehova, akimwomba amsaidie kusitawisha tamaa ya kuongea na wanashule wenzake. Alianza kutoa ushahidi wa vivi hivi shuleni, akawa na matokeo mazuri, na upesi akaanza kuongea na kila mtu aliyemjua. Alimalizia kwa kusema hivi: “Vijana hao wanahitaji na wanataka tumaini la wakati ujao, na Yehova anatutumia kuwasaidia.”

5 Majirani: Huenda tukawa na majirani au watu wengine tunaowafahamu ambao huudhika kwa sababu ya jinsi tunavyotambuliwa na kwa sababu ya itikadi zetu. Ikiwa waogopa wanachofikiria, jiulize hivi: ‘Je, wanajua kweli inayoongoza kwenye uhai udumuo milele? Naweza kufanya nini ili nifikie mioyo yao?’ Mwangalizi mmoja wa mzunguko aliona kwamba kunakuwa na matokeo mazuri majirani wanapohubiriwa kidogo-kidogo kwa ukawaida. Mwombe sana Yehova akupe nguvu inayohitajiwa na hekima ya kuendelea kutafuta watu wenye mioyo minyoofu.—Flp. 4:13.

6 Tukishindwa na msongo usiofaa wa marika huenda hilo likafurahisha wapinzani, lakini je, kufanya hivyo kutawafaidi wao—au sisi? Yesu alipingwa na watu wa jamii yake mwenyewe. Hata alivumilia maneno makali ya ndugu zake wa kambo. Lakini alijua kwamba angewasaidia tu kwa kubaki mwaminifu katika mwendo ambao Mungu alikusudia. Hivyo basi, Yesu “[ali]vumilia maongezi yaliyo kinyume ya namna hiyo yenye kufanywa na watenda-dhambi dhidi ya masilahi yao wenyewe.” (Ebr. 12:2, 3) Twapaswa kufanya hivyo. Azimia kutimiza pendeleo lako la kuhubiri ujumbe wa Ufalme kwa njia bora zaidi uwezavyo. Kwa kufanya hivyo, “utajiokoa wewe mwenyewe na wale wakusikilizao pia.”—1 Tim. 4:16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki