Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/02 uku. 4
  • Unganishweni Pamoja kwa Upatano

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Unganishweni Pamoja kwa Upatano
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari Zinazolingana
  • Umoja wa Kikristo Unamletea Mungu Utukufu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Ni Nini Kinacholeta Umoja wa Kweli Miongoni mwa Wakristo?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • “Yehova Mmoja” Anaikusanya Familia Yake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Unaweza Kuchangiaje Kuimarisha Umoja Wetu wa Kikristo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 7/02 uku. 4

Unganishweni Pamoja kwa Upatano

1 Je, ni mara ngapi umestaajabia ubuni wenye ustadi wa mwili wa binadamu? (Zab. 139:14) Kila kiungo cha mwili hushirikiana na viungo vingine. Neno la Mungu hulinganisha kutaniko la Kikristo na mwili wenye viungo vinavyotenda kwa upatano. Chini ya Kichwa, ambaye ni Kristo, washiriki wote wa kutaniko ‘wameunganishwa pamoja kwa upatano na kufanywa washirikiane kupitia kila kiungo ambacho hupa kile kihitajiwacho.’ (Efe. 4:16a) Kwa hiyo, Yehova anaweza kutumia watu wake waliounganishwa ili kutimiza kazi zake za ajabu.

2 Washiriki wa kutaniko la karne ya kwanza walitenda “kwa umoja” ili kutimiza mahitaji ya kiroho na ya kimwili ya kila mmoja. (Mdo. 2:44-47) Kwa msaada wa Yehova, kwa umoja walikabili na kushinda upinzani mkali. (Mdo. 4:24-31) Walitangaza habari njema ya ujumbe wa Ufalme popote walipokwenda, wakisambaza habari njema katika sehemu zote za dunia zilizojulikana wakati huo. (Kol. 1:23) Nyakati za kisasa, kutaniko la Kikristo limeungana kutimiza kazi hiyohiyo kwa kiwango kikubwa zaidi. Ni mambo gani yanayosaidia kuleta umoja huo?

3 Waunganishwa na Mafundisho ya Mungu: Ulimwenguni pote, tumeunganishwa na ibada yetu. Hilo lawezekanaje? Twatambua njia ya Yehova inayoonekana ya kuandaa ‘chakula cha kiroho kwa wakati ufaao.’ (Mt. 24:45) Pia twathamini “zawadi [zikiwa] wanadamu” ambao ametupa wawe walimu katika kutaniko. Tunapokubali kwa unyenyekevu mipango ya Yehova ya kutulisha kiroho, uelewevu wetu wa Neno la Mungu hukua na kutuchochea sisi sote tuwe na tamaa ya kumwiga Yesu tukiwa wanafunzi wake. Lazima twendelee kujifunza Neno la Mungu, tukijitahidi kwa bidii ‘kufikia umoja katika imani.’ (Efe. 4:8, 11-13) Je, unachangia umoja wetu wa kiroho kwa kusoma Biblia kila siku?

4 Kuunganishwa na Ushirika wa Kikristo: Upendo hutuunganisha ili tushirikiane kwa ukaribu kwenye mikutano ya Kikristo. Kwenye mikutano hiyo, sisi ‘hufikiriana.’ (Ebr. 10:24, 25) Hiyo yatia ndani kutozingatia mambo ya juujuu lakini kuwajua ndugu zetu, kuwaona kama Yehova anavyowaona, kuwa wao ni wenye thamani. (Hag. 2:7) Tunaposikiliza maelezo yao ya imani, tunazidi kuwapenda na umoja wetu unaimarishwa. Je, wengine wanajua kuwa unahudhuria mikutano ya kutaniko kwa ukawaida?

5 Wafanyakazi Wenzetu Katika Utumishi wa Shambani: Kuhubiri habari njema pamoja na waamini wenzetu hutuunganisha kufanya mapenzi ya Mungu. Mtume Paulo alithamini ‘wafanyakazi wenzake kwa ajili ya ufalme wa Mungu.’ (Kol. 4:11) Kusimulia mambo yaliyoonwa na kusaidiana tunapohubiri hutusaidia kutimiza utume wetu wa Kikristo na kuimarisha umoja wetu.—Kol. 3:14.

6 Nguvu Yenye Kuunganisha ya Roho Takatifu: Yehova hutupatia roho yake tunapojitahidi kufanya mapenzi yake. Hiyo hutusaidia kutofikiria makosa ya wengine na kuishi pamoja kwa umoja. (Zab. 133:1) Hutuchochea “kushika umoja wa roho katika kifungo chenye kuunganisha cha amani.” (Efe. 4:3) Kila mmoja wetu anaweza kuendeleza upatano uliopo miongoni mwa watu wa Mungu kwa kuonyesha matunda ya roho takatifu tunaposhughulika na wenzetu.—Gal. 5:22, 23.

7 Kutumikia pamoja kwa umoja chini ya uongozi wa Kristo “hutokeza ukuzi wa mwili ili kujijenga huo wenyewe katika upendo.” (Efe. 4:16b) Zaidi ya hilo, humtukuza Yehova, “Mungu apaye amani.”—Rom. 16:20.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki