Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/04 uku. 1
  • ‘Enyi Washikamanifu Wote, Mpendeni Yehova’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Enyi Washikamanifu Wote, Mpendeni Yehova’
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari Zinazolingana
  • “Endeleeni Kufanya Hivi kwa Kunikumbuka Mimi” Ukumbusho wa Kifo cha Yesu Utakuwa Aprili 2
    Huduma ya Ufalme—2007
  • Wasaidie Wengine Wafaidike na Fidia
    Huduma ya Ufalme—2006
  • Yehova Hubariki Jitihada Zetu za Kuadhimisha Ukumbusho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2023
  • “Endeleeni Kufanya Hivi”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 3/04 uku. 1

‘Enyi Washikamanifu Wote, Mpendeni Yehova’

Kifo cha Yesu Kitaadhimishwa Aprili 4

1 Miaka iliyopita, wakati nchi ya Ukrainia ilipokuwa ikitawaliwa na Wakomunisti, akina ndugu walichunguzwa na wenye mamlaka hasa Mlo wa Jioni wa Bwana ulipokuwa ukikaribia. Walitaka kujua mahali watakapokutania. Kila mwaka, hilo lilikuwa tatizo kwa kuwa wenye mamlaka waliweza kukisia tarehe ya mwadhimisho. Ndugu wangefanya nini? Nyumba ya dada mmoja ilikuwa na chumba cha chini kilichojaa maji. Kwa kuwa wenye mamlaka hawangetarajia watu kukutana humo, akina ndugu walijenga jukwaa juu ya maji hayo yaliyofika magotini. Ingawa iliwabidi kuchutama kwa sababu dari ilikuwa fupi, waliadhimisha Ukumbusho kwa furaha bila kusumbuliwa na yeyote.

2 Jitihada za ndugu zetu wa Ukrainia za kutii agizo la kuadhimisha kifo cha Yesu zilionyesha wazi kwamba wanampenda Mungu. (Luka 22:19; 1 Yoh. 5:3) Mifano hiyo inaweza kututia moyo kila mara tunapokabiliana na vizuizi maishani mwetu na kutusaidia kuazimia kuhudhuria na kuadhimisha Mlo wa Jioni wa Bwana mnamo Aprili 4. Kwa kufanya hivyo, tunaonyesha kwamba tuna maoni kama ya mtunga-zaburi aliyeimba hivi: “Enyi washikamanifu wake wote, mpendeni Yehova.”—Zab. 31:23.

3 Wasaidie Wengine Wazidi Kumpenda Mungu: Upendo wetu kwa Mungu hutuchochea pia tuwaalike wengine waadhimishe kifo cha Yesu pamoja nasi. Nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Februari ilimtia moyo kila mmoja wetu kuandika orodha ya watu tunaopanga kuwaalika kwenye Ukumbusho. Je, unajitahidi kumwalika kila mtu katika orodha yako? Waeleze kinaganaga umuhimu wa Ukumbusho. Unaweza kuwatia moyo kuhudhuria kwa kuwakumbusha kwa njia ya kirafiki siku na saa ya Ukumbusho, na hata unaweza kuandamana nao ikiwa inafaa.

4 Jitahidi sana kuwasalimu na kuwakaribisha wote wanaohudhuria. Utawasaidiaje wampende Yehova zaidi? Uwe tayari kujibu maswali yao. Uwe tayari kuwatolea funzo la Biblia ikiwezekana. Waalike kwenye mikutano ya kila juma ya kutaniko. Wazee hasa wanapaswa kuzungumza na Wakristo wasiotenda ambao wamehudhuria. Wanaweza kupanga kuwatembelea na kuwatia moyo warudie utendaji wao wakitumia mambo yaliyozungumziwa katika hotuba ya Ukumbusho.—Rom. 5:6-8.

5 Kuzidisha Upendo Wetu Wenyewe kwa Yehova: Kutafakari zawadi ya fidia kunaweza kuzidisha upendo wetu kwa Yehova na Mwanaye. (2 Kor. 5:14, 15) Shahidi mmoja ambaye amekuwa akihudhuria Ukumbusho kwa miaka mingi alisema hivi: “Sisi hutazamia Ukumbusho kwa hamu. Ukumbusho huwa tukio la pekee zaidi kwetu kila mwaka. Miaka 20 iliyopita, nakumbuka jinsi nilivyothamini sana fidia nilipokuwa kwenye chumba cha maiti nikimtazama baba yangu mpendwa aliyekuwa amekufa. Kabla ya baba kufa sikuthamini kamwe fidia. Ama kweli, nilijua maandiko yote kuhusu fidia na hata niliweza kuyafafanua! Lakini nilipogundua kwamba kifo ni halisi, moyo wangu ulifurahi sana nilipofikiria jinsi ambavyo fidia hiyo yenye thamani itakavyotufaidi.”—Yoh. 5:28, 29.

6 Tarehe ya mwadhimisho wa mwaka huu inapokaribia, tayarisha moyo wako kwa ajili ya tukio hilo. (2 Nya. 19:3) Tafakari usomaji wa pekee wa Biblia wa Ukumbusho ulioonyeshwa katika kijitabu Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2004 na Kalenda ya 2004. Wengine hufurahia kusoma sura ya 112-116 ya kitabu Mtu Mkuu Zaidi. Wengine hufanya utafiti zaidi wakitumia vifaa vilivyotolewa na mtumwa mwaminifu na mwenye busara. (Mt. 24:45-47) Sisi sote tunaweza kusali kwa bidii na kushukuru kwa zawadi ya fidia. (Zab. 50:14, 23) Naam, katika majira haya ya Ukumbusho sisi sote na tuendelee kutafakari upendo wa Yehova kwetu na tutafute njia za kuonyesha kwamba tunampenda.—Marko 12:30; 1 Yoh. 4:10.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki