Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/06 uku. 8
  • Wafundishe Wapole Kutembea Katika Njia ya Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wafundishe Wapole Kutembea Katika Njia ya Mungu
  • Huduma ya Ufalme—2006
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi ya Kuwasaidia Wengine Washike Amri za Kristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • “Basi, Nendeni Mkafanye Wanafunzi”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Daima Kaza Uangalifu kwa Kufundisha Kwako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • “Mkafanye Wanafunzi . . . Kuwafundisha”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2006
km 3/06 uku. 8

Wafundishe Wapole Kutembea Katika Njia ya Mungu

1 Wanafunzi wa Kristo wa karne ya kwanza walisemwa kuwa walikuwa wa “Ile Njia.” (Mdo. 9:2) Ukristo wa kweli unatia ndani njia yote ya maisha ya mtu. (Met. 3:5, 6) Kwa hiyo, tunapoongoza mafunzo ya Biblia, haitoshi tu kuwafundisha wanafunzi ujuzi sahihi wa mafundisho ya Biblia. Tunapaswa pia kuwasaidia watembee katika njia ya Yehova.—Zab. 25:8, 9.

2 Kumpenda Yehova na Yesu: Bila shaka ni vigumu kwa wanadamu wasio wakamilifu kufanya fikira, mtazamo, usemi, na mwenendo wao upatane na mapenzi ya Mungu! (Rom. 7:21-23; Efe. 4:22-24) Hata hivyo, kumpenda Mungu na Mwana wake huwachochea wapole wajitahidi kufanya hivyo. (Yoh. 14:15; 1 Yoh. 5:3) Tunawezaje kuwasaidia wanafunzi wetu wa Biblia wasitawishe upendo wa aina hiyo?

3 Msaidie mwanafunzi wako afahamu utu wa Yehova. Ndugu mmoja alieleza hivi: “Watu hawawezi kumpenda mtu wasiyemjua, hivyo tangu mwanzoni mwa funzo, mimi huwafundisha jina la Mungu kutoka katika Biblia, nami hutafuta fursa za kukazia sifa za Yehova.” Kuzungumzia mfano wa Yesu ni njia nzuri sana ya kufanya hivyo. (Yoh. 1:14; 14:9) Kwa kuongezea, tumia sanduku la kurudia mwishoni mwa kila sura ya kitabu Biblia Inafundisha kumsaidia mwanafunzi aige sifa zenye kupendeza za Mungu na Mwanaye.

4 Fundisha kwa Mfano: Tukiwa walimu na viongozi, sisi huwaonyesha wengine kwa matendo yetu kinachomaanishwa na kutembea katika njia ya Mungu. (1 Kor. 11:1) Kwa mfano, wanafunzi wengi wa Biblia hawajazoea kuzungumza na watu wasiowajua ili kuwaeleza imani yao. Kwa hiyo, huenda ukahitaji subira na ustadi ili kuwasaidia wasitawishe upendo, imani, na ujasiri unaohitajika ili kushiriki katika kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi. (2 Kor. 4:13; 1 The. 2:2) Tamaa yetu ya kuwasaidia wanafunzi wetu itatuchochea kuandamana nao na kuwategemeza wanapopiga hatua za kwanza katika huduma ya Kikristo.

5 Mfano wako unaweza kuwafundisha wanafunzi katika sehemu nyingine muhimu za maisha ya Kikristo. Unapowatembelea wagonjwa au kuwasalimu wengine katika mikutano ya kutaniko, wanajionea upendo. (Yoh. 15:12) Unaposhiriki katika kusafisha Jumba la Ufalme au kuwasaidia wengine, unawafundisha jinsi ambavyo wanaweza kutumika. (Yoh. 13:12-15) Wanapoona kwamba unadumisha maisha sahili, wanatambua kinachomaanishwa na ‘kuendelea kuutafuta kwanza ufalme.’—Mt. 6:33.

6 Kazi ya kuwafundisha wengine Neno la Mungu na kufanya wanafunzi inahitaji jitihada nyingi. Lakini ni shangwe iliyoje kuwaona wapole ‘wakiendelea kutembea katika kweli’!—3 Yoh. 4.

[Maswali ya Funzo]

1. Ni nini kinachohusika katika kufanya wanafunzi?

2. Ni nini kinachoweza kumchochea mwanafunzi wa Biblia kufuata amri za Mungu?

3. Tunaweza kuwasaidiaje wanafunzi wampende Yehova na Yesu?

4. (a) Kwa nini wanafunzi wengi huona kuhubiri kuwa jambo gumu? (b) Tunaweza kuwasaidiaje wanafunzi kupiga hatua za kwanza katika huduma ya Kikristo?

5. Mfano mzuri unaweza kuwasaidiaje wanafunzi waone yale yanayohusika katika kufuata amri za Mungu?

6. Kuwasaidia wapole wamtumikie Yehova huwa na matokeo gani?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki