Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/08 uku. 4
  • Wafundishe Wengine Kumpenda Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wafundishe Wengine Kumpenda Yehova
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Habari Zinazolingana
  • Mpende Mungu Anayekupenda
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • “Lazima Umpende Yehova Mungu Wako”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Mwige Yesu—Fundisha Kwa Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Usiruhusu Upendo Wako Upoe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 9/08 uku. 4

Wafundishe Wengine Kumpenda Yehova

1. Ni nini kinachowafanya watu fulani wavutiwe na Yehova?

1 Je, unakumbuka mara ya kwanza uliposikia kumhusu Yehova? Ni jambo gani ambalo lilikuvuta kwake? Watu wengi wenye moyo mnyoofu watakwambia kwamba walivutiwa na Muumba wetu walipojifunza kuhusu sifa zake za ajabu, hasa huruma zake na upendo wake.—1 Yoh. 4:8.

2, 3. Tunaweza kutumiaje kitabu Biblia Inafundisha kuwasaidia wanafunzi wa Biblia wazidi kumpenda Yehova?

2 “Huyu Ndiye Mungu Wetu”: Kitabu Biblia Inafundisha kinakazia upendo wa Yehova na uhitaji wa kuwa na uhusiano wa kibinafsi pamoja naye. Tunaweza kutumiaje kitabu hicho kuwasaidia wengine wazidi kumpenda Mungu? Tunapozungumzia hoja fulani mpya, tunaweza kuwauliza maswali ya kujichunguza, kama vile: “Kweli hii inakufundisha nini kumhusu Yehova?” au “Hoja hii inaonyeshaje kwamba Yehova ndiye Baba bora zaidi?” Kufundisha kwa njia hiyo kunaweza kumsaidia mwanafunzi kuanza kuwa na uhusiano wa kudumu pamoja na Yehova.

3 Tunapowasaidia wanafunzi wa Biblia kuthamini kwamba ni pendeleo kujifunza kumhusu Mungu wa pekee wa kweli na aliye hai, watakubaliana na maneno ya Isaya kwamba “huyu ndiye Mungu wetu.” (Isa. 25:9) Tunapofafanua Neno la Mungu, tunahitaji kukazia jinsi ambavyo wanadamu watabarikiwa wakati makusudi ya Yehova yatakapotimizwa kupitia serikali yake ya kifalme chini ya Kristo Yesu.—Isa. 9:6, 7.

4, 5. Kumpenda Yehova kunamaanisha nini?

4 Mambo Yanayoonyesha Kwamba Mtu Anampenda Yehova: Tunajua kwamba kumpenda Yehova kwa moyo, nafsi, na akili yote kunahusisha mengi zaidi ya kuwa na hisia zenye nguvu kumwelekea Mungu. Ni lazima tujipatanishe na kushikamana na njia yake ya kufikiri. (Zab. 97:10) Mtu anaonyesha kwamba anampenda Mungu kwa kutii amri zake zote na kuendelea kufanya “matendo matakatifu ya mwenendo na vitendo vya ujitoaji-kimungu,” hata wakati wa majaribu na upinzani.—2 Pet. 3:11; 2 Yoh. 6.

5 Inafurahisha kufanya mapenzi ya Mungu kwa sababu tunampenda. (Zab. 40:8) Ni lazima mwanafunzi wa Biblia aelewe kwamba amri zote za Mungu zinawaletea watumishi Wake faida za kudumu. (Kum. 10:12, 13) Mtu anapoishi kupatana na mwongozo wa Yehova, anaonyesha kwamba anathamini sana kazi Zake zote za ajabu. Msaidie mwanafunzi kuelewa kwamba kutembea katika njia za Yehova za uadilifu kutamsaidia kuepuka matatizo na maumivu mengi.

6. Ni baraka gani ambazo mtu anaweza kupata kwa sababu ya kumpenda Yehova?

6 Baraka kwa Wale Wanaompenda Mungu: Yehova anawajali sana watu wanyenyekevu wanaompenda, na anawafunulia “mambo mazito ya Mungu.” (1 Kor. 2:9, 10) Kwa kuwa wana ujuzi huo wa makusudi ya Yehova, wana maoni yaliyo wazi kuhusu wakati ujao na wana tumaini hakika. (Yer. 29:11) Wale wanaompenda Yehova wanapata fadhili zake zisizo na kifani. (Kut. 20:6) Wana tumaini la uzima wa milele kwa sababu Mungu anawapenda sana.—Yoh. 3:16.

7. Unahisije kuhusu kuwafundisha wengine wampende Yehova?

7 Kadiri tunavyopata ujuzi kumhusu Baba yetu wa mbinguni, ndivyo tunavyokuwa na mengi zaidi ya kuwaeleza wengine. (Mt. 13:52) Ni pendeleo kubwa kama nini kuwafundisha wengine, na hasa watoto wetu, kumpenda Yehova! (Kum. 6:5-7) Acheni sisi, na wanafunzi wetu wa Biblia, tuendelee kububujikwa na sifa tunapojionea ‘wingi wa wema wa Yehova.’—Zab. 145:7.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki