HAZINA ZA NENO LA MUNGU | ZABURI 79-86
Ni Nani Mtu wa Maana Zaidi Katika Maisha Yako?
Inawezekana kwamba mtungaji wa Zaburi ya 83 alikuwa mzao wa Mlawi aliyeitwa Asafu, aliyeishi wakati mmoja na Mfalme Daudi. Zaburi hiyo iliandikwa katika kipindi ambacho mataifa yenye uadui yalikuwa tishio kwa watu wa Yehova.
Katika sala yake, mtunga-zaburi alikazia fikira jina la Yehova na enzi yake kuu badala ya usalama wake binafsi
Leo, watumishi wa Mungu wanaendelea kukabili mashambulizi mbalimbali. Kuvumilia kwetu kwa uaminifu humletea Yehova heshima
Yehova anataka tulijue jina lake
Tunapaswa kuonyesha kwa matendo kwamba Yehova ndiye Mtu wa maana zaidi katika maisha yetu