Kutumia wakati kujifunza Biblia na kutafakari
Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
AMKENI!
Swali: Je, Biblia imetoka kwa Mungu? Au ni kitabu chenye mawazo ya wanadamu?
Andiko: 2Ti 3:16
Toleo: Gazeti hili la Amkeni! linaeleza mambo matatu yanayothibitisha kwamba Biblia kwa kweli imetoka kwa Mungu.
FUNDISHA KWELI
Swali: Tunapaswa kuionaje zawadi ya uhai?
Andiko: Ufu 4:11
Kweli: Kwa kuwa uhai ni zawadi kutoka kwa Mungu, tunapaswa kuuheshimu. Hatuhatarishi uhai wetu na hatuwezi kuwaua kimakusudi wanadamu wenzetu. Tunathamini sana zawadi ya uhai.
NI NINI SIRI YA KUWA NA FAMILIA YENYE FURAHA?
Swali: Hebu ona swali lililo kwenye ukurasa wa kwanza wa trakti hii na majibu yaliyoonyeshwa. Una maoni gani?
Andiko: Lu 11:28
Toleo: Trakti hii inaonyesha faida ambazo familia yako inaweza kupata na kwa nini tuamini mambo ambayo Biblia inasema.
ANDIKA UTANGULIZI WAKO
Tumia mapendekezo yaliyoonyeshwa kutayarisha utangulizi wako