MAISHA YA MKRISTO
“Jaza Mkono Zawadi kwa Ajili ya Yehova”
Leo tunaweza kufanya nini ili ‘kuja tukiwa na zawadi mkononi kwa ajili ya Yehova”? (1Nya 29:5, 9, 14) Zifuatazo ni njia ambazo tunaweza kuchagua kutoa michango ya hiari ili kutegemeza kazi ya Mashahidi wa Yehova katika eneo letu na ulimwenguni pote.
MICHANGO INAYOTOLEWA MTANDAONI AU KUTIWA NDANI YA MASANDUKU YA MICHANGO INATEGEMEZA:
KAZI YA ULIMWENGUNI POTE
kujenga na kuendesha ofisi za tawi na ofisi za utafsiri
shule za kitheokrasi
watumishi wa pekee wa wakati wote
kutoa msaada wakati wa misiba
kuchapisha, kutayarisha video, na kutokeza machapisho ya kielektroni
MICHANGO YA KUTANIKO LENU
gharama za kutaniko, kama vile umeme, maji, na kadhalika na pia udumishaji wa Jumba la Ufalme
maazimio yanayofanywa na kutaniko ili kutuma michango kwenye ofisi ya tawi kwa ajili ya:
ujenzi wa Majumba ya Ufalme na ya Kusanyiko ulimwenguni pote
Mpango wa Kutoa Msaada Ulimwenguni Pote
utendaji mwingine wa ulimwenguni pote
MAKUSANYIKO
Michango inayotolewa katika kusanyiko la eneo husaidia kutegemeza kazi ya ulimwenguni pote. Vivyo hivyo, gharama zinazohusiana na makusanyiko ya eneo, ya pekee, na ya kimataifa zinatoka kwenye michango ya kazi ya ulimwenguni pote.
Michango inayotolewa katika mzunguko inatumiwa kukodi, kuendesha, na kudumisha maeneo ya kufanyia kusanyiko la mzunguko na kushughulikia gharama nyingine. Mzunguko unaweza kupitisha azimio la kutoa mchango wa pesa za ziada kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote ya Mashahidi wa Yehova.