Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb21 Januari uku. 11
  • Chagua Kumtumikia Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Chagua Kumtumikia Yehova
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2021
  • Habari Zinazolingana
  • Ubatizo​—Lengo Muhimu!
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Ubatizo​—Takwa kwa Wakristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Kutimiza Matakwa ya Ubatizo wa Kikristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Ubatizo na Uhusiano Wako Pamoja na Mungu
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2021
mwb21 Januari uku. 11
Njia inayowakilisha barabara inayoongoza katika kumtumikia Yehova. Ishara zilizowekwa njiani zinawakilisha hatua za kuchukua yaani, kujifunza Biblia, kuhudhuria mikutano, kuhubiri, na kubatizwa.

Umefikia hatua gani katika barabara inayoongoza kwenye ubatizo?

MAISHA YA MKRISTO

Chagua Kumtumikia Yehova

Ikiwa wewe ni kijana Mkristo au mwanafunzi wa Biblia, je, una lengo la kubatizwa? Kwa nini ni muhimu kubatizwa? Kujiweka wakfu na kubatizwa kutakusaidia kuwa na uhusiano wa pekee na Yehova. (Zb 91:1) Kuchukua hatua hizo, huongoza kwenye wokovu. (1Pe 3:21) Unaweza kufanya nini ili kufikia hatua hizo?

Jihakikishie kwamba hii ndiyo kweli. Unapokuwa na maswali, fanya utafiti. (Ro 12:2) Tambua unahitaji kufanya mabadiliko gani, kisha uyafanye ukiwa na nia ya kumtumikia Yehova. (Met 27:11; Efe 4:23, 24) Sikuzote sali kwake ili kumwomba msaada. Uwe na uhakika kwamba Yehova atakuimarisha na kukutegemeza kupitia roho yake takatifu yenye nguvu. (1Pe 5:10, 11) Jitihada zako si za bure. Kumtumikia Yehova ndiyo njia bora zaidi ya maisha!—Zb 16:11.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA BARABARA INAYOONGOZA KWENYE UBATIZO, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Watu fulani wameshinda vizuizi gani ili wabatizwe?

  • Unaweza kusitawishaje imani inayohitajika ili kujiweka wakfu kwa Yehova?

  • Ni nini ambacho kimewachochea watu fulani kuchukua hatua zinazohitajika ili kufikia ubatizo?

  • Wale wanaochagua kumtumikia Yehova wanapata baraka gani?

  • Wakfu na ubatizo unamaanisha nini?

Mwishoni mwa hotuba ya ubatizo, msemaji atawaomba wale wanaotaka kubatizwa wasimame na kujibu maswali mawili yafuatayo kwa sauti inayosikika waziwazi:

Je, umetubu dhambi zako, ukajiweka wakfu kwa Yehova, na kukubali njia yake ya wokovu kupitia Yesu Kristo?

Je, unaelewa kwamba ubatizo wako unakutambulisha kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova anayeshirikiana na tengenezo la Yehova?

Kujibu maswali hayo ni “tangazo la hadharani” la kwamba wale wanaotaka kubatizwa wana imani katika fidia na kwamba wamejiweka wakfu kwa Yehova kwa moyo wote.—Ro 10:9, 10.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki