MAISHA YA MKRISTO
Hadi Ufufuo Utakapokuwa Halisi
Mpendwa wetu anapokufa, tunafarijiwa na tumaini la ufufuo. Hata hivyo, dhambi na kifo ni kama kifuniko kinachotulemea sisi sote. (Isa 25:7, 8) Hiyo ni sababu moja kwa nini “uumbaji wote unaendelea kuugua pamoja na kuwa katika maumivu pamoja.” (Ro 8:22) Tunaweza kukabilianaje na kifo cha mpendwa hadi wakati ambapo ufufuo utakuwa halisi? Neno la Mungu lina kanuni zinazoweza kutusaidia.
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA MPENDWA WAKO ANAPOKUFA, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Ni uchungu gani ambao Danielle, Masahiro, na Yoshimi wamekabili?
Mapendekezo matano yanayofaa yaliwasaidiaje?
Ni nani Chanzo kikuu cha faraja?—2Ko 1:3, 4