Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w20 Machi uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Habari Zinazolingana
  • Mambo Yaliyotarajiwa na Kuhofiwa Kuhusu Polisi
    Amkeni!—2002
  • “Wakaita Pamoja Sanhedrini”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Kwa Nini Ni Muhimu Kuwa na Polisi?
    Amkeni!—2002
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
w20 Machi uku. 31
Polisi wa Kiyahudi wa hekaluni wamewakamata wanaume wawili kwa mwongozo wa wapinzani wa kidini.

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Polisi wa Kiyahudi wa hekaluni walikuwa nani? Walifanya kazi gani?

Mojawapo ya majukumu mengi yaliyoshughulikiwa na watu wa kabila la Lawi ambao hawakuwa makuhani lilikuwa kutumikia katika utumishi unaofanana na wa maofisa wa polisi. Kikosi hicho kilikuwa chini ya uongozi wa kapteni wa hekalu. Philo, mwandishi Myahudi anafafanua hivi majukumu ya maofisa hao: “Baadhi yao [Walawi] wamepewa kazi ya kusimama kwenye miingilio wakiwa walinda malango, wengine kwenye [eneo la hekalu] mbele ya mahali patakatifu ili kumzuia yeyote asiyeruhusiwa na sheria kuingia mahali hapo, iwe anafanya hivyo kimakusudi au la. Wengine wanalinda doria kwa zamu wakipokezana usiku na mchana.”

Kikosi hicho cha polisi kilikuwa tayari kulitumikia baraza la Sanhedrini. Hicho ndicho kikosi pekee cha Wayahudi kilichobeba silaha ambacho Waroma walikiruhusu kufanya kazi.

Kulingana na msomi Joachim Jeremias, “Maneno ya kushutumu ambayo Yesu alitamka alipokamatwa, kwamba siku baada ya siku alikuwa hekaluni akifundisha lakini hakukamatwa (Mt. 26:55), yanaeleweka waziwazi zaidi ikiwa polisi wa Hekaluni ndio waliokuja kumkamata.” Msomi huyo anaamini kwamba wale waliotumwa ili kumkamata Yesu hapo awali walikuwa pia polisi wa hekaluni. (Yoh. 7:32, 45, 46) Baadaye, maofisa pamoja na kapteni wao walitumwa na Sanhedrini wawalete wanafunzi wa Yesu mbele yao, na inaonekana kwamba walihusika wakati mtume Paulo alipokokotwa nje ya hekalu.—Mdo. 4:1-3; 5:17-27; 21:27-30.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki