Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w22 Desemba uku. 14
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • Habari Zinazolingana
  • Yehova Alikuwa “Mwokoaji” Katika Nyakati za Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Tegemea Roho ya Mungu Unaposhughulika na Mabadiliko ya Maisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • “Unifundishe Kufanya Mapenzi Yako”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Na Tulikweze Jina la Yehova Pamoja
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
w22 Desemba uku. 14

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Je, mtunga zaburi Daudi alikuwa akitia chumvi au kusema maneno yasiyo sahihi alipoandika kwamba angelisifu jina la Mungu “milele,” kama vile ilivyoandikwa kwenye Zaburi 61:8?

Mfalme Daudi anaimba huku akipiga kinubi.

Hapana. Mambo ambayo Daudi aliandika ni ya kweli na sahihi.

Fikiria mambo aliyoandika kwenye mstari huo na mistari inayofanana na mstari huo: “Nitaliimbia sifa jina lako milele ninapotimiza nadhiri zangu siku baada ya siku.” “Ninakusifu, Ee Yehova Mungu wangu, kwa moyo wangu wote, nami nitalitukuza jina lako milele.” “Nitalisifu jina lako milele na milele.”—Zab. 61:8; 86:12; 145:1, 2.

Daudi alipoandika maneno hayo hakuwa akifikiri kwamba hatakufa kamwe. Alijua Yehova alikuwa amesema kwamba dhambi ya wanadamu ingetokeza kifo, na Daudi alikiri kwamba alikuwa mtenda dhambi. (Mwa. 3:3, 17-19; Zab. 51:4, 5) Alijua kwamba hata wanaume ambao walikuwa na kibali cha Mungu, kama vile Abrahamu, Isaka, na Yakobo, walikuwa wamekufa. Na Daudi alijua kwamba hatimaye yeye pia angekufa. (Zab. 37:25; 39:4) Lakini maneno yake yanayopatikana kwenye Zaburi 61:8 yalionyesha tamaa na azimio lake la kumsifu Mungu milele, yaani, katika maisha yake yote.​—2 Sam. 7:12.

Baadhi ya mambo ambayo Daudi aliandika ni mambo ambayo alijionea maishani, kama tunavyoona kwenye utangulizi wa Zaburi 18, 51, na 52. Kwenye Zaburi 23, Daudi ambaye yeye pia alikuwa mchungaji, alimfafanua Yehova kuwa mchungaji ambaye huandaa mwongozo, burudisho, na ulinzi. Hilo lilimfanya Daudi atamani kumtumikia Mungu ‘sikuzote za maisha yake.’​—Zab. 23:6.

Pia, kumbuka kwamba Yehova ndiye aliyemwongoza Daudi kuandika maneno hayo. Mambo aliyoandika yalitia ndani unabii kuhusu mambo ambayo yangetokea baadaye. Kwa mfano, kwenye Zaburi 110, Daudi alitaja kuhusu wakati ambao Bwana wake ‘angeketi kwenye mkono wa kuume wa Mungu’ huko mbinguni na kupokea mamlaka kubwa. Ili afanye nini? Ili awatiishe maadui wa Mungu na ‘atekeleze hukumu dhidi ya mataifa’ duniani. Daudi alikuwa babu ya Masihi, ambaye angetawala akiwa mbinguni na ambaye angekuwa “kuhani milele.” (Zab. 110:1-6) Yesu alithibitisha kwamba unabii ulio kwenye Zaburi 110 ulimhusu na kwamba ungetimizwa wakati ujao.​—Mt. 22:41-45.

Naam, Daudi aliongozwa na roho kuandika kuhusu wakati wake na pia wakati ujao ambapo angefufuliwa na angefurahia kumsifu Yehova milele. Hilo linatusaidia kuona kwamba andiko la Zaburi 37:10, 11, 29 linaweza kueleweka kama ufafanuzi wa hali ambazo zilikuwepo katika Israeli la kale na pia hali ambazo zitakuwepo ulimwenguni pote wakati ujao Mungu atakapotimiza ahadi zake.​—Tazama fungu la 8 kwenye makala “Utakuwa Pamoja Nami Katika Paradiso” kwenye gazeti hili.

Basi, Zaburi 61:8 na mistari mengine kama hiyo inaonyesha kwamba Daudi alitaka kumsifu Yehova katika Israeli la kale hadi wakati ambapo angekufa. Na pia, inaonyesha mambo ambayo Daudi ataweza kufanya wakati ujao Yehova atakapomfufua.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki