Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 184
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Ndoa?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Ndoa?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Mungu ameweka viwango gani kwa ajili ya ndoa?
  • Mungu ana maoni gani kuhusu kutengana na kutalikiana?
  • Je, ni lazima ndoa iandikishwe kisheria ili ikubaliwe na Mungu?
  • Biblia inasema mume na mke wana majukumu na wajibu gani?
  • Je, Mungu anatarajia kwamba lazima wenzi wa ndoa wawe na watoto?
  • Biblia inaweza kuisaidiaje ndoa yangu?
  • Jinsi ya Kufanikiwa Katika Ndoa ya Kikristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Ndoa​—Zawadi Kutoka kwa Mungu
    Jinsi ya Kudumu Katika Upendo wa Mungu
  • Jinsi ya Kufanikisha Ndoa
    Amkeni!—2011
  • Jenga Ndoa Imara na Yenye Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 184
Wenzi wa ndoa wakifurahi kuwa pamoja huku wakila kiamsha-kinywa.

Biblia Inasema Nini Kuhusu Ndoa?

Jibu la Biblia

Baada ya kumuumba mwanamume na mwanamke wa kwanza, Mungu aliwaunganisha katika ndoa. Alianzisha ndoa iwe muungano wa pekee kati ya mwanamume na mwanamke na hivyo kufanyiza mazingira yanayofaa ya kuwa na familia.—Mwanzo 1:27, 28; 2:18.

Mungu anataka wenzi wa ndoa wawe na furaha. (Methali 5:18) Katika Biblia, ameandaa viwango kwa ajili ya ndoa na kanuni zinazoweza kusaidia ndoa ifanikiwe.

Katika makala hii

  • Mungu ameweka viwango gani kwa ajili ya ndoa?

  • Mungu ana maoni gani kuhusu kutengana na kutalikiana?

  • Je, ni lazima ndoa iandikishwe kisheria ili ikubaliwe na Mungu?

  • Biblia inasema mume na mke wana majukumu na wajibu gani?

  • Je, Mungu anatarajia kwamba lazima wenzi wa ndoa wawe na watoto?

  • Biblia inaweza kuisaidiaje ndoa yangu?

  • Mistari ya Biblia kuhusu ndoa

Mungu ameweka viwango gani kwa ajili ya ndoa?

Tangu mwanzo, Mungu alikusudia ndoa iwe muungano kati ya mume mmoja na mke mmoja. (Mwanzo 2:24) Mungu anachukia ndoa ya wake wengi, matendo ya ngono kati ya watu wa jinsia moja, au watu kuishi pamoja bila kufunga ndoa. (1 Wakorintho 6:9; 1 Wathesalonike 4:3) Yesu aliwafundisha wafuasi wake kutii kiwango ambacho Mungu aliweka kwa ajili ya ndoa.—Marko 10:6-8.

Kwa maoni ya Mungu, ndoa ni muungano wa kudumu. Mwanamume na mwanamke wanapofunga ndoa wanaahidi kwamba watakuwa washikamanifu na kukaa pamoja muda wote wa maisha yao. Mungu anawatarajia watimize ahadi hiyo.—Marko 10:9.

Mungu ana maoni gani kuhusu kutengana na kutalikiana?

Kuna pindi ambazo huenda mwenzi mmoja akalazimika kuwa mbali na mwenzake, kama vile mmoja wao anapohitaji kusafiri ili kushughulikia dharura ya familia. Hata hivyo, Biblia haipendekezi kutengana kwa sababu ya matatizo ya ndoa. Badala yake, inawahimiza wenzi wa ndoa walio na matatizo ya ndoa wajitahidi kupatana.—1 Wakorintho 7:10.

Uzinzi ndio msingi pekee wa kimaandiko wa kutalikiana. (Mathayo 19:9) Hivyo, mume na mke wakiamua kutengana au kutalikiana kwa sababu nyingine yoyote isipokuwa uzinzi, hakuna yeyote kati yao aliye huru Kimaandiko kumchumbia mtu mwingine au kufunga ndoa naye.—Mathayo 5:32; 1 Wakorintho 7:11.

Je, ni lazima ndoa iandikishwe kisheria ili ikubaliwe na Mungu?

Mungu anatarajia Wakristo watii sheria za serikali kuhusu ndoa. (Tito 3:1) Wenzi wa ndoa wanapoandikisha ndoa yao kisheria, wanaonyesha heshima kwa mamlaka za serikali na kwa kiwango cha Mungu kwamba ndoa ni muungano wa kudumu.a

Biblia inasema mume na mke wana majukumu na wajibu gani?

  • Majukumu ya wote wawili. Waume na wake wanapaswa kutendeana kwa upendo na heshima. (Waefeso 5:33) Kila mmoja anapaswa kushughulikia mahitaji ya ngono ya mwenzake kwa njia yenye upendo na kuepuka aina zote za ukosefu wa uaminifu. (1 Wakorintho 7:3; Waebrania 13:4) Ikiwa wana watoto, mume na mke wana jukumu la kusaidiana kuwalea.—Methali 6:20.

    Mama akimsaidia binti yake kufanya kazi za shule huku baba akikatakata mboga karibu nao.

    Biblia haisemi kihususa jinsi wenzi wa ndoa wanavyopaswa kugawana majukumu yanayohusu kazi ya kimwili na kazi za nyumbani. Wanapaswa kuamua pamoja ni nini kitakachofaa familia yao.

  • Jukumu la mume. Biblia inasema kwamba “mume ni kichwa cha mke wake.” (Waefeso 5:23) Yeye ni kichwa katika maana kwamba anapaswa kuongoza familia yake na kufanya maamuzi ambayo yatamnufaisha mke wake na watoto wake.

    Wenzi wa ndoa wakisoma Biblia pamoja nyumbani na kufurahia viburudisho.

    Anapaswa kuhakikisha kwamba mahitaji yao ya kimwili, kihisia, na kiroho yanashughulikiwa. (1 Timotheo 5:8) Anaonyesha kwamba anathamini sifa na uwezo wa mke wake kwa kufanya kazi pamoja naye na kwa kufikiria kwa makini maoni na hisia zake anapofanya maamuzi. (Methali 31:11, 28) Biblia inasema kwamba mume anapaswa kushughulikia majukumu yake kwa upendo.—Wakolosai 3:19.

  • Jukumu la mke. Biblia inasema kwamba “mke anapaswa kumheshimu sana mume wake.” (Waefeso 5:33) Mke anapoheshimu jukumu ambalo Mungu amemkabidhi mume wake, Mungu anafurahi.

    Mume na mke wakizungumzia mambo yanayohusu pesa pamoja.

    Jukumu la mke ni kuwa msaidizi wa mume wake, kumsaidia kufanya maamuzi mazuri, na kuunga mkono ukichwa wake. (Mwanzo 2:18) Biblia inamsifu mke anayetimiza jukumu lake muhimu katika ndoa.—Methali 31:10.

Je, Mungu anatarajia kwamba lazima wenzi wa ndoa wawe na watoto?

Hapana. Zamani Mungu aliamuru baadhi ya waabudu wake wazae watoto. (Mwanzo 1:28; 9:1) Lakini agizo hilo haliwahusu Wakristo leo. Yesu hakuamuru kamwe kwamba wafuasi wake wapate watoto. Pia, wanafunzi wake wa karne ya kwanza hawakusema kwamba lazima wenzi wa ndoa wapate watoto. Wenzi wa ndoa hujiamulia wenyewe ikiwa watazaa watoto.

Biblia inaweza kuisaidiaje ndoa yangu?

Biblia ina kanuni zinazoweza kuwasaidia wenzi wa ndoa kuanzisha ndoa yao vizuri. Pia, kanuni za Biblia zinaweza kuwasaidia wenzi wa ndoa kuepuka au kushinda hali ngumu.

Kanuni za Biblia zinaweza kuwasaidia wenzi wa ndoa . . .

  • kuonyesha upendo wa kweli.—1 Wakorintho 13:4-7; Wakolosai 3:14.

  • kushughulikia kutoelewana.—1 Wakorintho 10:24.

  • kuwa wasikilizaji wazuri.—Yakobo 1:19.

  • kuonyesha heshima.—Waroma 12:10.

  • kusamehe.—1 Petro 4:8.

  • kuwa washikamanifu.—Marko 10:9.

  • kuwa na subira.—Waefeso 4:2, 3.

  • kufanya kazi pamoja.—Mhubiri 4:9.

  • kuimarisha uhusiano wao.—Wimbo wa Sulemani 8:7.

a Ili kupata habari kuhusu maoni ya Biblia kuhusiana na ndoa za kimila au za kikabila, ona Mnara wa Mlinzi la Oktoba 15, 2006, ukurasa wa 21, fungu la 12.

Mistari ya Biblia kuhusu ndoa

Methali 18:22: “Anayepata mke mwema amepata kitu chema.”

Maana: Biblia inaonyesha kwamba kufunga ndoa ni jambo jema.

Malaki 2:15: “Usimtendee kwa hila mke wa ujana wako.”

Maana: Mungu anawataka waume na wake wawe waaminifu na kutendeana kwa heshima, hata baada ya kuishi katika ndoa kwa miaka mingi.

Marko 10:9: “Kile ambacho Mungu ameunganisha, mtu yeyote asikitenganishe.”

Maana: Mungu alikusudia ndoa iwe muungano wa kudumu.

Waebrania 13:4: “Ndoa na iheshimiwe kati ya wote.”

Maana: Wenzi wa ndoa wanapaswa kuthamini sana ndoa yao na kutia jitihada ili kuilinda.

1 Wakorintho 7:28: “Wale [wanaofunga ndoa] watakuwa na dhiki katika mwili wao.”

Maana: Hakuna ndoa kamilifu; wenzi wa ndoa wanahitaji kushirikiana ili kushinda changamoto zinazojitokeza.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki