Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwhf makala 11
  • Kijana Anapotenda Jambo Linalokufanya Uache Kumwamini

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kijana Anapotenda Jambo Linalokufanya Uache Kumwamini
  • Msaada kwa Ajili ya Familia
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Je, kijana wangu ni mwasi?
  • Vipi ikiwa kijana wangu amenidanganya?
  • Ni nani anayepaswa kulaumiwa?
  • Ninaweza kumsaidiaje kijana wangu ili nimwamini tena?
  • Jinsi ya Kumwekea Kijana Wako Sheria
    Amkeni!—2013
  • Unawezaje kuzungumza na kijana wako bila kubishana naye?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Jinsi ya Kuwasiliana na Kijana Wako
    Amkeni!—2013
  • Jinsi ya Kumtia Nidhamu Kijana Wako
    Amkeni!—2013
Pata Habari Zaidi
Msaada kwa Ajili ya Familia
ijwhf makala 11
Baba na mama waliokatishwa tamaa na kijana wao.

MSAADA KWA AJILI YA FAMILIA | KULEA WATOTO

Kijana Anapotenda Jambo Linalokufanya Uache Kumwamini

Vijana fulani hufika nyumbani baada ya saa ambazo walipangiwa na wazazi wao. Wengine huwaambia wazazi wao uwongo na labda hata kutoka nyumbani bila ruhusa ili wakawe na rafiki zao. Unaweza kufanya nini kijana wako anapofanya jambo linalokufanya uache kumwamini?

  • Je, kijana wangu ni mwasi?

  • Vipi ikiwa kijana wangu amenidanganya?

  • Ni nani anayepaswa kulaumiwa?

  • Ninaweza kumsaidiaje kijana wangu ili nimwamini tena?

  • Wazazi wanasema nini?

Je, kijana wangu ni mwasi?

Si lazima awe mwasi. Biblia inasema hivi: “Ujinga umefungwa katika moyo wa kijana,” na mara nyingi vijana huthibitisha ukweli wa maneno hayo. (Methali 22:15, maelezo ya chini) Dakt. Laurence Steinberg anaandika hivi: “Vijana hufanya maamuzi fulani haraka-haraka na ya kipumbavu. Tarajia tu kwamba watafanya makosa.”a

Vipi ikiwa kijana wangu amenidanganya?

Usijiambie kwamba lengo la kijana wako ni kukosa kukutii. Utafiti unaonyesha kwamba vijana wanajali sana maoni ya wazazi kuwahusu, hata ikiwa hawaonyeshi hilo. Huenda kijana wako anahuzunishwa na jambo alilofanya na kwamba amekufanya uache kumwamini, hata ikiwa haonyeshi hisia hizo wazi.b

Picha: 1. X-ray inayoonyesha mfupa wa mguu uliovunjika. 2. Mguu uliofungwa plasta. 3. Mwanamume akitembea baada ya mguu kupona.

Mfupa uliovunjika, unapounga, unaweza kuwa na nguvu tena. Ni hivyo pia mtu anapotenda kwa njia inayokufanya uache kumwamini

Ni nani anayepaswa kulaumiwa?

  • Je, ni mazingira yake? Biblia inasema hivi: “Msipotoshwe. Kushirikiana na watu wabaya huharibu tabia nzuri.” (1 Wakorintho 15:33) Ni kweli kwamba marafiki wanaweza kuwaathiri sana vijana. Mbali na hilo, wao huathiriwa na hali nyingine kama vile mitandao ya kijamii na matangazo ya kibiashara. Pia, vijana hawana uzoefu maishani, kwa hiyo, wanaweza kufanya maamuzi yasiyofaa kwa urahisi. Bila shaka, wanapaswa kuwajibika kwa maamuzi wanayofanya ili wakomae na kuwa watu wazima wanaotegemeka.

  • Je, ni kosa langu? Huenda ukajiuliza ikiwa ulikuwa mgumu sana hivi kwamba kijana wako akatenda kwa njia isiyofaa. Au huenda pindi fulani ukafikiri kwamba ulimwendekeza sana kijana wako na kumpa uhuru mwingi sana. Badala ya kukazia fikira ulichangiaje tatizo lake, fikiria jinsi unavyoweza kumsaidia.

Ninaweza kumsaidiaje kijana wangu ili nimwamini tena?

  • Dhibiti jinsi unavyotenda. Huenda kijana wako anatarajia ukasirike. Kwa nini usitende kwa njia tofauti? Zungumza na kijana wako kwa utulivu ujue ni nini kilichomchochea afanye makosa. Je, ni udadisi? Je, alikuwa amechoshwa? Alikuwa mpweke? Alitamani kuwa na rafiki zake? Hakuna sababu yoyote kati ya hizi inayotetea jambo alilofanya, lakini inaweza kukusaidia—na kumsaidia kijana wako—kuelewa kilichomfanya atende kama alivyofanya.

    Kanuni ya Biblia: ‘Uwe mwepesi wa kusikia, si mwepesi wa kusema, si mwepesi wa hasira.’—Yakobo 1:19.

  • Msaidie kijana wako atafakari kilichotokea. Uliza maswali kama vile, Umejifunza nini kutokana na ulichofanya? Wakati ujao ungefanya nini kwa njia tofauti na ulivyofanya wakati huu? Maswali kama hayo yanaweza kumsaidia kijana wako kujifunza jinsi ya kufanya maamuzi yanayofaa.

    Kanuni ya Biblia: “Karipia, kemea, himiza, kwa subira yote na ustadi wa kufundisha.”—2 Timotheo 4:2.

  • Msaidie aelewe kwamba matendo yake yana madhara. Adhabu yoyote inayotolewa inapaswa kupatana na kosa lililofanywa ili kijana ajifunze kutokana nalo. Kwa mfano, kijana wako akitumia gari bila idhini yako, unaweza kumzuia asitumie gari kwa muda fulani.

    Kanuni ya Biblia: “lolote analopanda mtu, ndilo atakalovuna pia.”—Wagalatia 6:7.

  • Kazia fikira jinsi ya kumsaidia umwamini tena. Ni kweli kwamba hilo huchukua muda. Hata hivyo, kijana wako anapaswa kujua kwamba baada ya muda, anaweza kuanza kuaminika tena. Hakikisha kwamba anajua jambo hilo. Akihisi kwamba hutawahi kumwamini tena, huenda akavunjika moyo.

    Kanuni ya Biblia: “Msiwe mkiwakasirisha watoto wenu, ili wasivunjike moyo.”—Wakolosai 3:21.

Bablu ya taa.

Dokezo: Mwekee kijana wako mfano kwa kumwomba msamaha wakati ambapo wewe unakosea au kufanya uamuzi usiofaa.

Wazazi wanasema nini

Joseph na Lisa.

“Ikiwa wazazi si wenye kutegemeka, watoto wao hawawezi kujifunza kuwa wenye kutegemeka. Lakini, watoto wanapoona kwamba wazazi wanaweka mfano mzuri wa kuwa wenye kuaminika, watataka kuaminika pia na watajihisi vizuri wanapofanya hivyo.”—Joseph, akiwa na mke wake, Lisa.

Karyn na Daniel.

“Kusitawisha uhusiano mzuri na watoto wanapokuwa wachanga kutakusaidia katika ile miaka migumu ya utineja. Pia wazazi wanahitaji kujifunza kuwapa vijana uhuru zaidi hatua kwa hatua, na kuweka wazi mipaka wanayoweka. Kijana anapohisi kwamba mzazi wake anajaribu kumwelewa na kumpa uhuru zaidi, hatatenda kwa njia itakayomfanya akose kuaminika.”—Karyn, akiwa na mume wake, Daniel.

Pitio: Kijana Anapotenda Jambo Linalokufanya Uache Kumwamini

  • Dhibiti jinsi unavyotenda. Zungumza na kijana wako kwa utulivu ujue ni nini kilichomchochea afanye makosa.

  • Msaidie kijana wako atafakari kilichotokea. Uliza maswali kama vile, Umejifunza nini kutokana na ulichofanya? Wakati ujao ungefanya nini kwa njia tofauti na ulivyofanya wakati huu?

  • Msaidie aelewe kwamba matendo yake yana madhara. Adhabu yoyote inayotolewa inapaswa kupatana na kosa lililofanywa ili kijana ajifunze kutokana nalo.

  • Kazia fikira jinsi ya kumsaidia umwamini tena. Kijana wako akihisi kwamba hutawahi kumwamini tena, huenda akavunjika moyo.

a Kutoka kwenye kitabu You and Your Adolescent.

b Habari iliyo katika makala hii inawafaa vijana wa kiume na wa kike pia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki