Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwyp makala 109
  • Je, Nibatizwe?—Sehemu ya 1: Maana ya Ubatizo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Nibatizwe?—Sehemu ya 1: Maana ya Ubatizo
  • Vijana Huuliza
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ubatizo ni nini?
  • Kujiweka wakfu kunamaanisha nini?
  • Kwa nini ubatizo ni muhimu?
  • Je, Uko Tayari Kubatizwa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Ubatizo​—Lengo Muhimu!
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Vijana Je, Mko Tayari Kubatizwa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Ubatizo​—Takwa kwa Wakristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
Pata Habari Zaidi
Vijana Huuliza
ijwyp makala 109
Kijana akibatizwa katika kidimbwi kwenye kusanyiko la Mashahidi wa Yehova.

VIJANA HUULIZA

Je, Nibatizwe?—Sehemu ya 1: Maana ya Ubatizo

Kila mwaka, vijana wengi wanaolelewa na Mashahidi wa Yehova hubatizwa. Je, unafikiria kuchukua hatua hiyo? Ikiwa ndivyo, kwanza unahitaji kuelewa maana ya kujiweka wakfu na kubatizwa.

  • Ubatizo ni nini?

  • Kujiweka wakfu kunamaanisha nini?

  • Kwa nini ubatizo ni muhimu?

  • Vijana wenzako wanasema nini

  • Maoni yasiyo sahihi na mambo hakika

Ubatizo ni nini?

Ubatizo unaotajwa katika Biblia unahusisha kuzamishwa kabisa ndani ya maji—wala si kunyunyiziwa maji—jambo lililo na maana ya pekee.

  • Kuzamishwa ndani ya maji wakati wa ubatizo ni tangazo la hadharani la kwamba umeacha maisha ya kufanya mapendezi yako mwenyewe.

  • Kuinuliwa kutoka ndani ya maji kunaonyesha kwamba umeanza maisha mapya ukiwa umekazia fikira kufanya mapenzi ya Mungu.

Kwa kubatizwa, unaonyesha hadharani kwamba unatambua Yehova ana mamlaka ya kuweka viwango vya mema na mabaya, na unatangaza rasmi kwamba umeahidi kwa hiari kuishi kulingana na matakwa yake.

Jambo la kufikiria: Kwa nini ufikirie kutangaza hadharani kwamba unataka kumtii Yehova katika maisha yako yote? Ona 1 Yohana 4:19 na Ufunuo 4:11.

Kujiweka wakfu kunamaanisha nini?

Kabla ya kubatizwa, unapaswa kujiweka wakfu kwa Yehova faraghani. Jinsi gani?

Katika sala yako ya kibinafsi, unamwambia Yehova kwamba unaahidi kumtumikia milele na kwamba utafanya mambo anayotaka hata hali iweje na hata watu wengine waamue kufanya nini.

Ubatizo ni tangazo la hadharani linaloonyesha kwamba ulijiweka wakfu. Unawaonyesha wengine kwamba umejikana mwenyewe na sasa wewe ni mali ya Yehova.—Mathayo 16:24.

Jambo la kufikiria: Kwa nini maisha yako yanakuwa bora zaidi unapokuwa mali ya Yehova? Ona Isaya 48:17, 18 na Waebrania 11:6.

Kwa nini ubatizo ni muhimu?

Yesu alisema kwamba wanafunzi wake walipaswa kubatizwa. (Mathayo 28:19, 20) Hivyo, ubatizo bado ni takwa kwa Wakristo. Kwa kweli, Biblia inasema kwamba ni muhimu mtu abatizwe ili aweze kuokolewa.—1 Petro 3:21.

Hata hivyo, nia yako ya kubatizwa inapaswa kuchochewa na upendo na uthamini wako kwa Yehova. Mtazamo wako unapaswa kuwa kama wa mtunga-zaburi aliyeandika hivi: “Nitamlipa Yehova nini kwa mema yote aliyonitendea? . . . Nami nitaliitia jina la Yehova. Nitamtimizia Yehova nadhiri zangu.”—Zaburi 116:12-14.

Jambo la kufikiria: Yehova amekufanyia mambo gani mema, na unaweza kumlipa jinsi gani? Ona Kumbukumbu la Torati 10:12, 13 na Waroma 12:1.

Vijana wenzako wanasema nini

Mijin.

“Wakfu unahusisha ahadi unayompa Yehova, na hilo ni jambo zito. Hata hivyo, kuna baraka nyingi ukiwa mtumishi wa Yehova aliyejiweka wakfu. Yeye anaweza kututunza kwa njia bora zaidi kuliko tunavyoweza kujitunza.”—Mijin.

Ember.

“Yehova ameshaonyesha kwamba anakupenda. Unapobatizwa unaonyesha kwamba unampenda sana. Kubatizwa ni pendeleo na baraka kubwa!”—Ember.

Julian.

“Uamuzi wa kujiweka wakfu kwa Mungu na kubatizwa ni uamuzi muhimu zaidi ambao mtu anaweza kufanya. Lakini hilo lisikuogopeshe. Ikiwa umejitayarisha na unafanya hivyo ukiwa na sababu nzuri, ni uamuzi bora zaidi utakaofanya.”—Julian.

Maoni yasiyo sahihi na mambo hakika

MAONI YASIYO SAHIHI — Watu wazima tu ndio waliokomaa vya kutosha ili kubatizwa.

JAMBO HAKIKA — Ukomavu unaonekana si kupitia umri bali kupitia jinsi mtu anavyompenda Yehova na utayari wake wa kumtii. Walipokuwa bado vijana, Yosefu, Samweli, na Yosia walionyesha ukomavu huo. Vijana wengi leo wanafanya hivyo.

Biblia inasema: “Mtoto hujulikana kwa matendo yake, kama tabia yake ni safi na ya unyoofu.”—Methali 20:11.

MAONI YASIYO SAHIHI — Ikiwa rafiki zako wanabatizwa, wewe pia unapaswa kubatizwa.

JAMBO HAKIKA — Uamuzi wa kujiweka wakfu na kubatizwa ni wa kibinafsi unaopaswa kufanywa kutoka moyoni. Si njia au desturi ambayo unapaswa uifanye unapofikia umri fulani kwa sababu tu wengine wamefanya hivyo au kwa sababu unafikiri kwamba wengine wanakutazamia ufanye hivyo.

Biblia inasema: “Watu wako watajitoa kwa hiari.”—Zaburi 110:3.

MAONI YASIYO SAHIHI — Ikiwa hujabatizwa, huwajibiki kutokana na matendo yako.

JAMBO HAKIKA — Unawajibika kwa Yehova si wakati unapobatizwa bali unapojua lililo jema na lililo baya machoni pake.

Biblia inasema: “Ikiwa mtu anajua jinsi ya kufanya yaliyo sawa na bado hayafanyi, hiyo ni dhambi kwake.”—Yakobo 4:17.

DOKEZO: Ikiwa daraka la kuwa Mkristo aliyejiweka wakfu na kubatizwa linaonekana kuwa lenye kulemea, kwa nini usichukue hatua ili kukabiliana na kushughulikia wasiwasi wako? Unaweza kufanya hivyo kwa kusoma Sura ya 37 katika kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2.

Muhtasari: Kwa nini ubatizo ni muhimu?

  • Yesu alisema kwamba lazima wanafunzi wake wabatizwe.

  • Ubatizo ni muhimu ili kupata wokovu.

  • Ni pendeleo kubwa kumtumikia Yehova ukiwa Mkristo aliyejiweka wakfu na kubatizwa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki