Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mrt makala 25
  • Ni Nani Atakayeiokoa Dunia?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Nani Atakayeiokoa Dunia?
  • Habari Zaidi
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Je, jitihada za wanadamu zitafanikiwa?
  • Sababu ya kuwa na tumaini
  • Je, Dunia Itaharibiwa?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Je, Wanadamu Wataiharibu Dunia Kabisa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Mungu Anaahidi Kwamba Dunia Yetu Itaokoka
    Amkeni!—2023
  • Zawadi ya Milele Kutoka kwa Muumba
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
Pata Habari Zaidi
Habari Zaidi
mrt makala 25
Msichana mdogo akimwagilia ua maji. Nyuma yake, viwanda vikichafua mazingira.

Ni Nani Atakayeiokoa Dunia?

Watu wengi wanahangaishwa na jinsi wanadamu wameiharibu dunia na uhai uliomo. Kulingana na wataalamu fulani wa mazingira, wanyama fulani wanakabili hatari ya kutoweka na unamnanamna wa uhai duniani uko hatarini kuliko wakati mwingine kwa sababu ya matendo ya wanadamu.

Je, wanadamu wataiangamiza dunia? Au je, watawahi kuishi kwa njia ambayo haiharibu mazingira?

Je, jitihada za wanadamu zitafanikiwa?

Wataalamu wengi wana uhakika kwamba wanadamu wanaweza kuilinda dunia na kuishi kwa upatano na vitu vya asili. Watafiti fulani wamesema kwamba ili jitihada za wanadamu zifanikiwe, lazima mabadiliko yafanywe katika nyanja kadhaa kwa wakati uleule. Mabadiliko hayo yanatia ndani:

  • Kuboresha jinsi ya kutunza ardhi, misitu, maeneo yenye maji mengi, na bahari.

  • Kutumia njia tofauti za ukulima na kutafuta vyanzo vipya vya nishati.

  • Kubadili jinsi chakula kinavyotokezwa na kusambazwa ili watu wale mazao ya mimea na kiasi kidogo tu cha nyama na samaki, na kwamba wanadamu wapunguze kiasi cha chakula wanachokula na wanachotupa.

  • Kukubali kwamba ubora wa maisha hautegemei kuwa na vitu vingi vya kimwili.

Una maoni gani? Je, inapatana na akili kutazamia serikali, biashara, na raia kushirikiana kwa njia kubwa hivyo? Au unafikiri kwamba inapatana na akili kutazamia kwamba pupa, ubinafsi, kutojali mambo ya wakati ujao kutazuia jitihada kama hizo?—2 Timotheo 3:1-5.

Sababu ya kuwa na tumaini

Biblia inatuhakikishia kwamba wakati ujao wa sayari yetu hauko hatarini. Inatueleza kwa nini jitihada za wanadamu hazitoshi kuiokoa dunia, na inafafanua ni mabadiliko gani yanayohitajika. Pia inafafanua jinsi mabadiliko hayo yatakavyofanyika.

Kwa nini jitihada za wanadamu pekee hazitoshi? Yehovaa Mungu aliiumba dunia na aliwapa wanadamu jukumu la kuitunza. (Mwanzo 1:28; 2:15) Wangefanikiwa kutimiza mgawo huo ikiwa tu wangemtegemea Muumba wao ili kupata mwongozo na kutii maagizo yake. (Methali 20:24) Hata hivyo, walimkataa Yehova na kujaribu kujiamulia mambo. (Mhubiri 7:29) Bila msaada, wanadamu hawana uwezo wa kuitunza dunia, na jitihada zozote wanazofanya haziwezi kufanikiwa sana.—Methali 21:30; Yeremia 10:23.

Badiliko ambalo lazima lifanyike. Mungu anakusudia kuwazuia wanadamu wasiiharibu dunia. (Ufunuo 11:18) Hataboresha serikali na jamii ya wanadamu wanaoiharibu sayari hii; badala yake, atawaondoa. (Ufunuo 21:1) Kwa sababu hiyo, Yehova anasema hivi: “Tazama! Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.”—Ufunuo 21:5.

Jinsi badiliko hilo litakavyotokea. Yehova ataondoa serikali za wanadamu na kusimamisha serikali mbinguni inayoitwa Ufalme wa Mungu. Serikali hiyo, inayoongozwa na Yesu Kristo, itatawala juu ya dunia yote.—Danieli 2:44; Mathayo 6:10.

Ufalme wa Mungu utawafundisha wanadamu jinsi ya kuishi kulingana na viwango vya Mungu vya uadilifu. Wanadamu watakapokubali kumsikiliza Muumba wao na kutii mwongozo wake, wataweza kuishi kwa upatano na vitu vya asili. (Isaya 11:9) Biblia inaonyesha jinsi serikali ya Mungu itakavyowawezesha raia wake kufurahia maisha bora, ambayo yatasaidia kuendeleza uhai duniani. Itafanya mambo yafuatayo:

  • Itawaandalia watu wote chakula.—Zaburi 72:16.

  • Itarekebisha mali za asili zilizoharibika.—Isaya 35:1, 2, 6, 7.

  • Itahakikisha wanadamu wanawatunza wanyama na wanyama hawatawaumiza wanadamu.—Isaya 11:6-8; Hosea 2:18.

  • Itazuia misiba ya asili.—Marko 4:37-41.

Unaweza kuwa na uhakika kwamba Ufalme wa Mungu utaleta mabadiliko hayo hivi karibuni. Ili kupata habari zaidi, ona makala yenye kichwa “Ufalme wa Mungu Utaanza Kutawala Dunia Lini?”

a Yehova ndilo jina la kibinafsi la Mungu.—Zaburi 83:18.

Tunaweza kufanya nini sasa ili kuonyesha kwamba tunaiheshimu sayari yetu?

Tunaposubiri Ufalme wa Mungu urekebishe kabisa matatizo ya mazingira yanayoikumba dunia, tunaweza kufanya mambo fulani sasa yanayoonyesha tunaiheshimu sayari yetu. Kwa mfano, tunaweza kuepuka kupoteza nishati, chakula, na mali nyingine za asili, na tunaweza kutii sheria kuhusu kutupa takataka kwa njia inayofaa ili zitumiwe tena.—Yohana 6:12, 13; Waroma 13:1, 5.

  • Brett.

    Brett ni mshauri wa mambo ya mazingira aliyestaafu. Elimu yake kuhusu ikolojia imemsaidia kutambua kuna Muumba ambaye atachukua hatua ili kuiokoa dunia. Soma simulizi lake.

  • Wafanyakazi wawili wakitazama majengo mapya ya Makao Makuu ya Ulimwenguni Pote ya Mashahidi wa Yehova.

    Njia moja ambayo Mashahidi wa Yehova huonyesha kwamba wanamheshimu Muumba wao ni kwa kutumia mbinu zinazolinda mazingira katika miradi yao mikubwa ya ujenzi. Ili kuona mambo ambayo wametimiza, tazama video yenye kichwa Eco-Friendly Design Brings Honor to Jehovah.

Mistari ya Biblia kuhusu dunia

Mwanzo 2:15: “Yehova Mungu akamchukua huyo mtu na kumweka katika bustani ya Edeni ili ailime na kuitunza.”

Maana: Mungu aliwapa wanadamu mgawo wa kuitunza dunia.

Mwanzo 1:28: “Mungu akawabariki, na Mungu akawaambia: ‘Zaeni, muwe wengi, muijaze dunia na kuitiisha, na mtawale samaki wa baharini na viumbe wanaoruka angani na kila kiumbe aliye hai anayetembea duniani.’”

Maana: Wanadamu walipewa jukumu la kuwatunza wanyama.

Isaya 45:18: “Kwa maana Yehova, Muumba wa mbingu, Mungu wa kweli, Yule aliyeiumba dunia, Yule aliyeitengeneza na kuifanya imara kabisa, ambaye hakuiumba tu bila sababu, lakini aliiumba ili ikaliwe, anasema hivi: ‘Mimi ni Yehova, wala hakuna mwingine.’”

Maana: Kusudi la Mungu kuelekea dunia halijabadilika. Itakaliwa na watu ambao watafanya kile ambacho alikusudia mwanzoni.

Zaburi 37:29: “Waadilifu wataimiliki dunia, nao wataishi humo milele.”

Maana: Wale wanaofuata viwango vya uadilifu vya Mungu watapata nafasi ya kuishi milele duniani.

Zaburi 98:6-8: “Pazeni sauti kwa ushindi mbele za Mfalme, Yehova. Bahari na ingurume na vitu vyote vinavyoijaza, dunia na wote wanaokaa humo. Mito na ipige makofi; milima na ipaze sauti pamoja kwa shangwe.”

Maana: Utawala wa Mungu utafanya mazingira yawe mazuri.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki