Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mrt makala 55
  • Dunia Inaharibiwa—Biblia Inasema Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Dunia Inaharibiwa—Biblia Inasema Nini?
  • Habari Zaidi
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kuharibiwa kwa mazingira kulitabiriwa
  • Wakati ujao wa sayari yetu uko salama
  • Je, Mataifa Yanaweza Kuepuka Msiba Mkubwa wa Hali ya Hewa?​—Biblia Inasema Nini?
    Habari Zaidi
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Wakati Wetu Ujao?
    Habari Zaidi
  • Viwango vya Juu Zaidi vya Joto Ulimwengu Pote—Biblia Inasema Nini?
    Habari Zaidi
  • Dunia Ina “Homa” Je, Kuna Tiba?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
Pata Habari Zaidi
Habari Zaidi
mrt makala 55
Picha ya Sayari Dunia kutoka angani. Nusu ya sayari inaonekana ina afya ilhali nusu nyingine imechomeka na kuharibika.

ENDELEA KUKESHA!

Dunia Inaharibiwa—Biblia Inasema Nini?

“Hivi karibuni sana kutakuwa na janga la hali ya hewa. Majiji makubwa yatafunikwa na maji. Joto linalopita kiasi. Dhoruba zenye kutisha. Ukosefu mkubwa wa maji. Kutoweka kwa jamii milioni moja za mimea na wanyama. Haya si mambo ya kuwaziwa au yaliyotiliwa chumvi. Ni mambo ambayo sayansi inatueleza yatatokea kwa sababu ya sera zetu za sasa za kuzalisha nishati.”​—Hotuba ya António Guterres, katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, kuhusu Jopo la Serikali Mbalimbali Kuhusu Mabadiliko ya Hali ya Hewa ripoti iliyotolewa Aprili 4, 2022.

“Wanasayansi wanatoa onyo kwamba katika miaka ijayo uharibifu unaotokana na mabadiliko ya hali ya hewa utaathiri mbuga zote 423 za wanyama [nchini Marekani], kwa kuwa zinaathiriwa zaidi na kupanda kwa joto ulimwenguni. Maonyo yanayotolewa tena na tena yanasikika kama yale tunayosoma katika Biblia: moto na mafuriko, kuyeyuka kwa miamba ya barafu, kupanda kwa kiwango cha maji baharini na mawimbi ya joto.”​—“Hali Mbaya ya Mafuriko Katika Yellowstone, Ishara ya Majanga Yatakayokuja,” The New York Times, Juni 15, 2022.

Je, matatizo ya hali mbaya ya mazingira ya dunia yanaweza kutatuliwa? Ikiwa ndivyo, ni nani atakayeyatatua? Chunguza kile ambacho Biblia inasema.

Kuharibiwa kwa mazingira kulitabiriwa

Biblia inasema kwamba Mungu ‘atawaharibu wale wanaoiharibu dunia.’ (Ufunuo 11:18) Mstari huo wa Biblia unatufundisha mambo matatu:

  1. 1. Matendo ya wanadamu yataharibu dunia kwa kiwango kikubwa.

  2. 2. Kutakuwa na mwisho kwa uharibifu unaoendelea duniani.

  3. 3. Mungu ndiye atakayetatua matatizo ya mazingira ya dunia, si wanadamu.

Wakati ujao wa sayari yetu uko salama

Biblia inasema kwamba “dunia inadumu milele.” (Mhubiri 1:4) Itakaliwa sikuzote.

  • “Waadilifu wataimiliki dunia, nao wataishi humo milele.”​—Zaburi 37:29.

Afya ya sayari yetu itarekebishwa kabisa.

  • “Nyika na nchi iliyokauka zitafurahi, na jangwa tambarare litashangilia na kuchanua maua kama zafarani.”​—Isaya 35:1.

Ili ujifunze kwa nini tunaweza kuwa na uhakika kwamba Mungu ataiokoa sayari yetu, soma makala “Ni Nani Atakayeiokoa Dunia?”

Ili uone kwa nini tunaweza kuwa na uhakika kuhusu wakati wetu ujao licha ya mabadiliko ya sasa ya hali ya hewa, soma makala yenye kichwa “Biblia Inasema Nini Kuhusu Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Wakati Wetu Ujao?”

Ili ujifunze jinsi Biblia inavyoweza kukusaidia na changamoto zinazosababishwa na matatizo ya mazingira, soma makala yenye kichwa “Je, Biblia Inaweza Kukusaidia Kukabiliana na Mabadiliko Makubwa ya Hali ya Hewa?”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki