Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 50
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Kujichanja Chale?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Kujichanja Chale?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Je, Nitiwe Alama ya Chanjo?
    Amkeni!—2003
  • Je, Nijichanje Chale?
    Vijana Huuliza
  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu
    Amkeni!—2004
  • Yaliyomo
    Amkeni!—2003
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 50

Biblia Inasema Nini Kuhusu Kujichanja Chale?

Jibu la Biblia

Biblia inataja kuhusu kuchanja chale mara moja tu katika kitabu cha Mambo ya Walawi 19:28, ambapo tunasoma hivi: “Msijitie alama ya chanjo.” Mungu aliwapa Waisraeli amri hiyo, na hivyo kuwafanya tofauti na watu waliowazunguka ambao walijitia alama za majina au maumbo ya miungu yao mwilini. (Kumbukumbu la Torati 14:2) Ingawa Sheria ambayo Mungu aliwapa Waisraeli haiwahusu Wakristo, tunapaswa kuzingatia kanuni inayotegemea sheria hiyo.

Je, Mkristo anapaswa kuchanja chale au kuuchora mwili wake?

Maandiko yafuatayo yanaweza kukusaidia ujue jinsi ya kutenda:

  • “Wajipambe kwa mavazi yenye . . . kiasi.”—1 Timotheo 2:9 New World Translation) Kanuni hiyo inawahusu wanaume na wanawake. Tunapaswa kuheshimu hisia za wengine na kuepuka kujifikiria wenyewe.

  • Wengine wanataka watambuliwe na watu au waonekane wako huru, ilhali wengine wanajichanja chale ili waonyeshe kwamba wanajiamini. Hata hivyo, Biblia inawatia moyo Wakristo ‘watoe miili yao kuwa dhabihu iliyo hai, takatifu, yenye kukubalika kwa Mungu, utumishi mtakatifu pamoja na nguvu zao za kufikiri.’ (Waroma 12:1) Tumia ‘nguvu zako za kufikiri’ kuamua ni kwa nini unataka kujichanja chale. Ikiwa unafanya hivyo kwa sababu unataka kufuata mtindo fulani au kuonyesha kwamba wewe ni mshiriki wa kikundi fulani, kumbuka kwamba kujichanja chale kuna madhara ya kudumu. Kuchunguza nia yako kunaweza kukusaidia kufanya uamuzi wa hekima.—Methali 4:7.

  • “Mipango ya mwenye bidii bila shaka huleta faida, lakini kila mtu anayetenda haraka-haraka bila shaka huuelekea uhitaji.” (Methali 21:5) Mara nyingi uamuzi wa kujichanja chale hufanywa bila kufikiria kwa uzito, na unaweza kuathiri uhusiano wako na wengine au kazi. Ni ghali sana kuchanja chale na kuna maumivu mengi sana unapoamua kuziondoa. Utafiti—kutia ndani biashara iliyositawi ya kuondoa watu chale—inaonyesha kwamba idadi kubwa ya watu waliojichanja chale wanajuta ni kwa nini walifanya hivyo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki