Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 80
  • Je, Wakati Wetu wa Kufa Umeamuliwa Mapema?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wakati Wetu wa Kufa Umeamuliwa Mapema?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Je! Wakati Ujao Wako Unaamuliwa na Ajali?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Mhubiri 3:11—“Amefanya Kila Kitu Kipendeze kwa Wakati Wake”
    Mistari ya Biblia Yafafanuliwa
  • Kuna Wakati wa Kila Kitu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Je, Matukio Yote Maishani Mwetu Yameshaamuliwa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 80
Mtu akiingizwa katika ambulansi huku wapita-njia wakimtazama

Je, Wakati Wetu wa Kufa Umeamuliwa Mapema?

Jibu la Biblia

Hapana, wakati wetu wa kufa haujaamuliwa mapema. Badala ya kuunga mkono imani ya kwamba maisha ya mwanadamu yameamuliwa mapema, Biblia inasema kwamba mara nyingi kifo husababishwa na ‘matukio yasiyotazamiwa.’​—Mhubiri 9:​11.

Je, Biblia haisemi kwamba kuna “wakati wa kufa”?

Ndiyo, Mhubiri 3:2 inasema kwamba kuna “wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa kilichopandwa.” Hata hivyo, muktadha wa mstari huu unaonyesha kwamba Biblia inazungumzia mambo ya kawaida yanayotukia katika maisha ya mwanadamu. (Mhubiri 3:​1-8) Mungu hajaweka wakati hususa wa mtu kufa kama tu ambavyo hamlazimishi mkulima kuanza kupanda wakati fulani hususa. Jambo linalokaziwa ni kwamba hatupaswi kukazia fikira mambo yasiyo ya maana hivi kwamba tunampuuza Muumba wetu.​—Mhubiri 3:​11; 12:​1, 13.

Uhai unaweza kurefushwa

Licha ya hali zisizotarajiwa maishani, kwa kawaida tunaweza kuishi muda mrefu tukifanya maamuzi ya hekima. Biblia inasema: “Sheria ya mwenye hekima ni chemchemi ya uzima, ili kumwepusha mtu na mitego ya kifo.” (Methali 13:14) Pia, Musa aliwaambia Waisraeli kwamba wangeweza ‘kufurahia maisha marefu’ ikiwa wangetii amri za Mungu. (Kumbukumbu la Torati 6:2, Neno—Biblia Takatifu) Tofauti na hilo, tunaweza kufupisha uhai wetu kwa kutenda isivyofaa au kipumbavu.​—Mhubiri 7:​17.

Hata hivyo, hatuwezi kuepuka kifo kwa sababu tu ya kuwa na hekima au kuwa waangalifu. (Waroma 5:​12) Lakini, hali hii itabadilika, kwa sababu Biblia inaahidi kwamba kuna wakati ambapo “kifo hakitakuwapo tena.”​—Ufunuo 21:4.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki