Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwyp makala 60
  • Ninapaswa Kujua Nini Kuhusu Kileo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ninapaswa Kujua Nini Kuhusu Kileo?
  • Vijana Huuliza
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Fikiria mambo yatakayotokea baada ya kunywa
  • Weka azimio
  • Wakristo Wanapaswa Kuwa na Maoni Gani Kuhusu Kileo?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Fuata Mwongozo wa Mungu Kuhusu Kileo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2023
  • Mtazamo Unaofaa Kuhusu Pombe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Jinsi ya Kudhibiti Matumizi ya Kileo
    Habari Zaidi
Pata Habari Zaidi
Vijana Huuliza
ijwyp makala 60
Kijana akipewa kileo na vijana wenzake

VIJANA HUULIZA

Ninapaswa Kujua Nini Kuhusu Kileo?

Biblia haikatazi kunywa kileo kwa kiasi ikiwa sheria ya nchi inakuruhusu kufanya hivyo. Hata hivyo, inakataza ulevi.​—Zaburi 104:15; 1 Wakorintho 6:​10.

Lakini utafanyaje ukilazimishwa kunywa kileo wakati sheria ya nchi au wazazi wako hawakuruhusu kufanya hivyo?

  • Fikiria mambo yatakayotokea baada ya kunywa

  • Weka azimio

  • Mambo ambayo vijana wenzako wanasema

Fikiria mambo yatakayotokea baada ya kunywa

Baadhi ya vijana wenzako huenda wanahisi kwamba kunywa kileo ni muhimu ili kufurahia maisha. Hata hivyo ni mambo gani yanayoweza kutokea baada ya kunywa kileo?

  • Mtu akiwa gerezani

    Matatizo ya kisheria. Ikitegemea mahali unapoishi, ikiwa unakunywa kileo wakati sheria ya nchi unayoishi hairuhusu kufanya hivyo, unaweza kutozwa faini, kufunguliwa mashtaka ya uhalifu, kupoteza leseni yako ya udereva, kutakiwa kufanya utumishi fulani wa kijamii, au kufungwa gerezani.​—Waroma 13:3.

  • Simu ya mkononi

    Itaharibu sifa zako nzuri. Kileo kinapunguza uwezo wa kujizuia. Ukilewa unaweza kusema au kufanya mambo ambayo utajutia baadaye. (Methali 23:31-​33) Katika kipindi hiki ambacho mitandao ya kijamii inatumiwa sana, matendo yako yanaweza kuchafua sifa zako nzuri kwa muda mrefu.

  • Mwanamke akitendewa vibaya

    Inadhoofisha ulinzi. Kileo kinaweza kufanya iwe rahisi kushambuliwa kimwili au kingono. Pia, unaweza kuongozwa kwa urahisi na ushawishi wa wengine, jambo linaloweza kufanya ujihatarishe zaidi au utende kinyume cha sheria.

  • Chupa tupu ya pombe

    Uraibu. Utafiti fulani unaonyesha kwamba kuna uwezekano mkubwa wa kuwa mraibu ikiwa ulianza kunywa kileo ukiwa na umri mdogo sana. Kunywa kileo ili kukabiliana na mikazo, upweke, au usumbufu kunaweza kufanya iwe vigumu sana kuacha zoea hilo.

  • Fuvu na mifupa iliyokingamana

    Kifo. Katika miaka ya karibuni, mtu mmoja hufa nchini Marekani kila baada ya dakika 52 kwa sababu ya dereva kuendesha gari akiwa amelewa. Katika kipindi cha miaka mitano, zaidi ya watu 1,500 walio chini ya umri wa miaka 21 walikufa kila mwaka kwa sababu ya aksidenti zilizosababishwa na ulevi. Hata ikiwa wewe hujanywa kileo, unajiweka katika mazingira hatari kama utakubali kuingia katika gari linaloendeshwa na mtu ambaye amelewa.

Weka azimio

Unaweza kuepuka hali ya hatari na gharama zinazotokana na kunywa kileo kupita kiasi ikiwa utaamua mapema mambo utakayofanya.

Kanuni ya Biblia: “Mtu mwerevu ni yule ambaye ameona msiba na kujificha.” (Methali 22:3) Si jambo la hekima kunywa kileo kabla ya kuendesha gari au kufanya kazi yoyote inayohitaji uwe mwangalifu sana.

Azimio: ‘Ikiwa nitachagua kunywa kileo, nitafanya hivyo wakati sheria ya nchi na hali zinaniruhusu.’

Kanuni ya Biblia: “Ninyi ni watumwa wake kwa sababu mnamtii yeye.” (Waroma 6:​16) Ikiwa unakunywa kileo kwa sababu rafiki zako wanakunywa, unawaruhusu wengine wakutawale. Ikiwa unakunywa ili kuepusha usumbufu au kukabiliana na mikazo, utashindwa kusitawisha ustadi wa kushughulikia matatizo yako.

Azimio: ‘Sitawaruhusu rafiki zangu wanilazimishe kunywa kileo.’

Kanuni ya Biblia: “Usiwe kati ya watu wanaokunywa divai mno.” (Methali 23:20) Ukishirikiana na watu wabaya, watadhoofisha azimio lako. Unajiweka kwenye hatari ikiwa unakuwa pamoja na watu wanaokunywa kileo kupita kiasi.

Azimio: ‘Sitashirikiana na watu wanaokunywa kileo kupita kiasi.’

Vijana Wenzako Wanasema Nini

Jordan

“Nilipokuwa shuleni, watu walijaribu kila mara kunishawishi ninywe kileo. Niliendelea kujikumbusha andiko la 1 Wakorintho 15:33, linalosema hivi: ‘Mashirika mabaya huharibu tabia nzuri.’”​—Jordan.

Jenna

“Ninajaribu kuepuka watu na hali zitakazonilazimisha kunywa kileo. Ninashukuru kwamba nina marafiki ambao wanafanya uamuzi mzuri inapohusu kunywa kileo.”​—Jenna.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki