Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwyp makala 61
  • Ninawezaje Kupata Faragha Zaidi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ninawezaje Kupata Faragha Zaidi?
  • Vijana Huuliza
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa nini wazazi wanaingilia faragha yangu?
  • Unaweza kufanya nini?
  • Je, Kuna Ubaya Wowote Kutaka Kuwa na Faragha?
    Amkeni!—2010
  • Kuna Ubaya wa Kutaka Faragha?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1
  • Saidia Tineja Wako Asitawi
    Siri ya Furaha ya Familia
  • Ninawezaje Kuwafahamu Wazazi Wangu Vizuri Zaidi?
    Amkeni!—2009
Pata Habari Zaidi
Vijana Huuliza
ijwyp makala 61
Baba akiangalia simu ya kijana wake, huku kijana huyo akiwa amekasirika

VIJANA HUULIZA

Ninawezaje Kupata Faragha Zaidi?

  • Kwa nini wazazi wanaingilia faragha yangu?

  • Unaweza kufanya nini?

  • Vijana wenzako wanasema nini

Kwa nini wazazi wanaingilia faragha yangu?

Wazazi wako wanasema kwamba wanakuhangaikia. Lakini kwa maoni yako, wanaingilia faragha yako. Kwa mfano:

  • Kijana anayeitwa Erin anasema hivi: “Baba yangu huchukua simu yangu, kisha hutaka nimpe nywila, halafu anasoma jumbe zote katika simu yangu. Nikikataa kumpa anafikiri kuna kitu ninachoficha.”

  • Denise, ambaye sasa ana umri wa miaka 20 hivi, anakumbuka jinsi mama yake alivyokuwa akichunguza simu yake. Anasema hivi: “Mama alikuwa akiangalia kila namba katika simu yangu na kutaka kujua ni ya nani, halafu angeniuliza mambo niliyozungumza na mtu huyo.”

  • Tineja anayeitwa Kayla anaeleza kwamba mama yake alisoma daftari lake aliloandika mambo yake ya kibinafsi. Anasema hivi: “Niliandika hisia zangu kuhusu mambo mbalimbali, na baadhi ya mambo niliyoandika yalimhusu mama! Baada ya tukio hilo, niliacha kuandika mambo ya kibinafsi.”

Jambo kuu: Wazazi wako wana wajibu wa kuhakikisha kwamba uko salama, na huwezi kudhibiti jinsi wanavyotimiza wajibu huo. Je, nyakati nyingine wanavuka mipaka? Labda. Jambo la kupendeza ni kwamba kuna mambo ambayo wewe unaweza kufanya ili usihisi kana kwamba faragha yako imeingiliwa.

Unaweza kufanya nini?

Sema mambo waziwazi. Biblia inatuhimiza “[tujiendeshe] kwa unyoofu katika mambo yote.” (Waebrania 13:18) Jitahidi kuwa mnyoofu kwa wazazi wako. Kadiri unavyokuwa mnyoofu na kusema mambo waziwazi, ndivyo watakavyokuruhusu uwe na faragha zaidi.

Jambo la kufikiria: Je, una rekodi nzuri ya unyoofu? Je, unachelewa kurudi nyumbani? unawaficha wazazi wako wasijue marafiki zako? unawaficha mambo unayofanya?

“Ninakubaliana na mambo ambayo wazazi wangu wananiagiza. Ninawaeleza waziwazi mambo yanayoendelea maishani mwangu. Ninawaeleza kila kitu wanachotaka kujua kunihusu, hivyo wananiamini zaidi na kunipa faragha.”​—Delia.

Uwe na subira. Biblia inasema hivi: “Endeleeni kuthibitisha ninyi wenyewe jinsi mlivyo.” (2 Wakorintho 13:5) Inachukua muda mrefu kujenga rekodi ya kuwa mwenye kutegemeka lakini kuna faida nyingi sana.

Jambo la kufikiria: Pindi fulani wazazi wako walikuwa matineja. Unafikiri jambo hilo linahusianaje na jinsi wanavyohangaikia maisha yako?

“Ninafikiri wazazi hukumbuka makosa waliyofanya na wasingependa watoto wao wafanye makosa hayo pia.”​—Daniel.

Elewa hisia zao. Jaribu kuona mambo kama wazazi wako wanavyoyaona. Biblia inasema kwamba mke mwenye uwezo “anaangalia shughuli za nyumba yake” na kwamba baba mzuri anawalea watoto wake “katika nidhamu na mwongozo wa akilini wa Yehova.” (Methali 31:27; Waefeso 6:4) Hakuna njia ya mkato ya kutimiza wajibu huo: wazazi wako wanahitaji kujihusisha katika maisha yako.

Jambo la kufikiria: Kwa kuwa wewe unajua mambo ambayo matineja wanapenda kufanya, ikiwa ungekuwa mzazi, je, wewe ungemruhusu mwana wako au binti yako awe na faragha kabisa, bila kujali anachofanya?

“Unapokuwa tineja, unaona kama wazazi wako ‘wanaingilia’ faragha yako. Lakini kwa kuwa sasa nimepita umri wa utineja, ninaweza kuelewa kwa nini wazazi wanahitaji kufanya hivyo. Inaonyesha jinsi wanavyokupenda.”​—James.

Vijana wenzako wanasema nini

Makenzie

“Wazazi wangu waliniruhusu niwe na faragha kwa kadiri fulani, lakini pia walinisaidia kujua kwamba wana jukumu la kunilinda. Kwa kuwa sasa nimepita umri wa utineja, ninafurahi wanaponisaidia na kunipa mwelekezo. Wazazi wanaendelea kukuhangaikia hata unapokuwa mtu mzima.”​—Makenzie.

Lauren

“Nilipokuwa tineja, kila siku mama angeingia chumbani kwangu na kuniuliza kuhusu mambo niliyokabili siku hiyo na jinsi nilivyohisi. Nilihisi kana kwamba anaingilia faragha yangu. Lakini sasa ninatambua kwamba alikuwa akinihangaikia sana na alitaka kutumia wakati wake kuzungumza nami.”​—Lauren.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki