Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwyp makala 75
  • Nifanye Nini Rafiki Yangu Akiniumiza?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Nifanye Nini Rafiki Yangu Akiniumiza?
  • Vijana Huuliza
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Unachopaswa kujua
  • Unachoweza kufanya
  • Mbona Rafiki Yangu Ananitendea Hivi?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
  • Kwa Nini Rafiki Yangu Aliniumiza?
    Amkeni!—2000
  • Kusamehe Kunamaanisha Nini?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Msiwakwaze “Hawa Wadogo”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
Pata Habari Zaidi
Vijana Huuliza
ijwyp makala 75
Msichana akimwambia mwenzake maneno ya kuumiza

VIJANA HUULIZA

Nifanye Nini Rafiki Yangu Akiniumiza?

  • Unachopaswa kujua

  • Unachoweza kufanya

  • Vijana wenzako wanasema nini

Unachopaswa kujua

  • Hakuna uhusiano wa wanadamu usio na matatizo. Kwa sababu si mkamilifu, huenda rafiki yako​—hata yule unayemwona kuwa rafiki wa karibu sana​—anaweza kufanya au kusema jambo ambalo litakuumiza. Bila shaka, wewe pia si mkamilifu. Kwa hiyo, ni jambo la haki kukumbuka wakati wewe ulipomuumiza mtu fulani.​—Yakobo 3:2.

  • Intaneti inaweza kufanya iwe rahisi kuumia. Kwa mfano, tineja anayeitwa David, alisema hivi: “Ukifungua mtandao wa kijamii na kuona picha za rafiki yako akiwa katika tafrija, unaweza kuanza kujiuliza kwa nini hukualikwa. Na kisha unaweza kuanza kuhisi umesalitiwa na ukahuzunika.”

  • Unaweza kujifunza kushughulikia tatizo.

Unachoweza kufanya

Jichunguze. Biblia inasema hivi: “Usikasirike haraka, kwa maana hasira ni dalili ya mjinga.”​—Mhubiri 7:9, maelezo ya chini.

“Wakati mwingine, baada ya muda unatambua kwamba jambo lililokukasirisha si kubwa sana.”​—Alyssa.

Jambo la kufikiria: Je, unakasirika haraka? Je, unaweza kujifunza kuvumilia zaidi udhaifu wa wengine?​—Mhubiri 7:​21, 22.

Fikiria faida za kusamehe. Biblia inasema hivi: “Ni fahari . . . kuachilia kosa.”​—Methali 19:11.

“Hata ikiwa una sababu ya kulalamika, ni jambo jema kusamehe kwa hiari, hilo halimaanishi kumfungia kinyongo na kufanya akuombe msamaha kila wakati kwa kosa ambalo umemsamehe. Ukisamehe, lifute kabisa kosa hilo.”​—Mallory.

Jambo la kufikiria: Je, ni jambo zito sana? Je, unaweza kusamehe ili kutafuta amani?​—Wakolosai 3:​13.

Kuingiza hewa yenye baridi kwenye chumba chenye joto

Kurudia-rudia kutaja makosa kila mara katika urafiki ni sawa na kurudia-rudia kufungua mlango na kuacha hewa yenye baridi iingie katika chumba chenye joto

Wafikirie wengine. Biblia inasema hivi: “Mkiangalia, si faida zenu wenyewe, bali pia faida za wengine.”​—Wafilipi 2:4.

“Ikiwa kuna upendo na heshima katika urafiki wenu, utakuwa na sababu yenye nguvu ya kusuluhisha matatizo haraka kwa sababu umejitoa katika urafiki wenu. Tayari umetumia jitihada nyingi katika urafiki huo, na usingependa kuupoteza.”​—Nicole.

Jambo la kufikiria: Je, kuna ukweli wowote katika maoni ya rafiki yako?​—Wafilipi 2:3.

Jambo kuu: Kujua jinsi ya kushughulika na hisia zenye kuumiza ni ustadi utakaokusaidia utakapokuwa mtu mzima. Kwa nini usijifunze kuwa na ustadi huo sasa?

Vijana wenzako wanasema nini

Kiana

“Si kila jambo linalohitaji kuzungumziwa. Ikiwa ninaweza kusuluhisha jambo fulani akilini mwangu na kusamehe, ninafanya hivyo. Hilo linaweza kudumisha amani, badala ya kuivuruga kwa kutaja makosa hata madogo sana.”​—Kiana.

Treigh

“Katika kila hali ninajiuliza hivi, ‘Je, jambo hili ni kubwa sana hadi lifanye nimpoteze rafiki?’ Kwa kweli katika kila kisa, jibu ni hapana.”​—Treigh.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki