Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 140
  • Yesu Huokoa—Jinsi Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yesu Huokoa—Jinsi Gani?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Jambo Ambalo Ni Lazima Tufanye Ili Tuokolewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Je, Mashahidi wa Yehova Wanaamini Kwamba Ni Wao Tu Watakaookolewa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Ni Lazima Tufanye Nini Tuokolewe?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Je, Biblia Inafundisha ‘Ukiokolewa, Umeokolewa Milele’?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 140
Yesu akiwa amezungukwa na watu wa rangi tofauti

Yesu Huokoa​—Jinsi Gani?

Jibu la Biblia

Yesu aliwaokoa wanadamu waaminifu alipotoa uhai wake kuwa dhabihu ya fidia. (Mathayo 20:28) Hivyo, Biblia inamwita Yesu “mwokozi wa ulimwengu.” (1 Yohana 4:​14) Pia inasema hivi: “Hakuna wokovu katika mwingine yeyote, kwa maana hakuna jina lingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu ambalo kupitia hilo tunaweza kuokolewa.”​—Matendo 4:​12.

Yesu ‘alionja kifo kwa ajili ya kila mtu’ anayemwamini. (Waebrania 2:9; Yohana 3:​16) Baada ya hapo, “Mungu alimfufua kutoka kwa wafu,” na Yesu akarudi mbinguni akiwa kiumbe wa roho. (Matendo 3:​15) Akiwa huko, Yesu anaweza “kuwaokoa kikamili wale wanaomkaribia Mungu kupitia yeye, kwa sababu sikuzote yuko hai ili kuwaombea.”​—Waebrania 7:​25.

Kwa nini tunahitaji Yesu atuombee?

Sisi sote ni watenda dhambi. (Waroma 3:​23) Dhambi hututenganisha na Mungu, nayo hutokeza kifo. (Waroma 6:​23) Lakini Yesu hutenda kama “wakili” kwa ajili ya wale wanaodhihirisha imani katika dhabihu yake ya fidia. (1 Yohana 2:1, maelezo ya chini) Anawaombea, akimsihi Mungu asikilize sala zao na kuwasamehe dhambi kwa msingi wa dhabihu ya kifo cha Yesu. (Mathayo 1:​21; Waroma 8:​34) Mungu anatenda kupatana na maombi hayo yanayotolewa na Yesu kwa sababu yanapatana na mapenzi Yake. Mungu alimtuma Yesu duniani ili “ulimwengu uokolewe kupitia kwake.”​—Yohana 3:​17.

Je, tunahitaji tu kumwamini Yesu ili tuokolewe?

Hapana. Ingawa lazima tumwamini Yesu ili tuokolewe, mengi zaidi yanahitajika. (Matendo 16:30, 31) Biblia inasema hivi: “Kama vile mwili bila roho umekufa, vivyo hivyo, imani bila matendo imekufa.” (Yakobo 2:​26) Ili tuokolewe tunapaswa:

  • Kujifunza kumhusu Yesu na Baba yake, Yehova.​—Yohana 17:3.

  • Kuwa na imani katika Yehova na Yesu.​—Yohana 12:44; 14:1.

  • Kuonyesha imani kwa kutii amri zao. (Luka 6:​46; 1 Yohana 2:​17) Yesu alifundisha kwamba si kila mtu anayemwita “Bwana” atakayeokolewa bali ni wale tu ‘wanaofanya mapenzi ya Baba yake aliye mbinguni.’​—Mathayo 7:​21.

  • Kuendelea kudhihirisha imani licha ya hali ngumu. Yesu alionyesha hilo ni muhimu aliposema: “Yule atakayevumilia mpaka mwisho ndiye atakayeokolewa.”​—Mathayo 24:13.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki