Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwyp makala 80
  • Ninaweza Kufanya Nini Ili Wazazi Wangu Waniamini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ninaweza Kufanya Nini Ili Wazazi Wangu Waniamini?
  • Vijana Huuliza
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Unachopaswa kujua
  • Unachoweza kufanya
  • Kwa Nini Wazazi Wangu Hawaniamini?
    Amkeni!—2008
  • Ninaweza Kupata Uhuru Zaidi Jinsi Gani?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1
  • 10 Uaminifu
    Amkeni!—2018
  • Kwa Nini Kuna Sheria Nyingi Sana?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
Pata Habari Zaidi
Vijana Huuliza
ijwyp makala 80
Msichana akiwaomba wazazi wake ruhusa ya kwenda matembezi na marafiki wake

VIJANA HUULIZA

Ninaweza Kufanya Nini Ili Wazazi Wangu Waniamini?

  • Unachopaswa kujua

  • Unachoweza kufanya

  • Vijana wenzako wanasema nini

Unachopaswa kujua

Watakuamini ikiwa utakuwa mwaminifu. Kutii sheria za wazazi ni kama kulipa deni. Una wajibu wa kuwatii wazazi wako, na kadiri unavyolipa deni, ndivyo unavyopata ‘mkopo’ (au uhuru) zaidi kutoka kwao. Kwa upande mwingine, usipokuwa mwaminifu, usishangae wazazi wakipunguza ‘kiwango chako cha kukopa.’

Unahitaji wakati mwingi ili uaminike. Unahitaji uwe na tabia ya kutimiza wajibu kabla ya wazazi wako kukupa uhuru zaidi.

SIMULIZI HALISI: “Nilipokuwa tineja, nilijua kabisa mambo ambayo wazazi walitaka nifanye, hivyo nilijifanya kana kwamba ninafanya mambo hayo hata ingawa kwa siri nilikuwa nikifanya mambo niliyotaka. Jambo hilo lilifanya wazazi wangu wasiniamini. Hatimaye, nilijifunza kwamba kuna njia moja tu ya kupata uhuru zaidi, yaani, kuwa mnyoofu. Unahitaji kuwa mwaminifu ili uaminike.”​—Craig.

Unachoweza kufanya

Sema kweli​—hata kama utapata adhabu. Kila mtu hufanya makosa, lakini kuficha makosa kwa kutumia uwongo (au kutosema habari fulani ili kuficha ukweli) kutafanya wazazi wako wasikuamini. Kwa upande mwingine, ukiwa na rekodi ya kuwa mnyoofu kabisa, wazazi wako wataona umekomaa vya kutosha kukiri makosa yako. Na huyo ndiye mtu anayeweza kuaminika.

“Si mara zote unapokosa kuaminika kwa sababu ya kufanya makosa, lakini mara nyingi unakosa kuaminika unapojaribu kuficha makosa.”​—Anna.

Biblia inasema: “Tunataka kujiendesha kwa unyoofu katika mambo yote.”​—Waebrania 13:18.

  • Jambo la kufikiria: Wazazi wako wanapokuuliza unaenda wapi na utafanya nini huko, je, unawaambia ukweli wote? Au wazazi wako wanapokuuliza ulienda wapi na ulikuwa ukifanya nini, je, unaficha baadhi ya habari ambazo wanahitaji kujua?

Wajibika. Tii sheria zote za nyumbani. Fanya kazi zako zote za nyumbani bila kukawia. Timiza ahadi zako kwa wakati. Fanya kazi zako za shule bila kushurutishwa. Usipitishe muda uliopangiwa kurudi nyumbani.

“Ikiwa wazazi wako wamekuruhusu uende matembezi na marafiki wako lakini wamekuomba urudi nyumbani saa 3:00 usiku, ukirudi nyumbani saa 4:30 usiku usitarajie wakati mwingine wakuruhusu uende tena matembezi na marafiki wako!”​—Ryan.

Biblia inasema: “Kila mtu ataubeba mzigo wake mwenyewe wa wajibu.”​—Wagalatia 6:5, maelezo ya chini.

  • Jambo la kufikiria: Una rekodi gani inapohusu kudumisha wakati, kumaliza kazi zako za nyumbani, na kutii sheria, hata zile ambazo huzipendi?

Uwe na subira. Ikiwa ulifanya jambo lililofanya uache kuaminiwa, itachukua muda kabla ya wazazi wako kukuamini tena. Uwe na subira.

“Nilivunjika moyo wazazi wangu walipokosa kunipa uhuru zaidi nilipofikia umri fulani. Sikutambua kwamba kuwa na umri mkubwa hakumaanishi kuwa mkomavu. Niliwaomba wazazi wangu wanipe nafasi ya kuwaonyesha kwamba ninatumainika. Ilichukua muda, lakini nilifanikiwa. Nilitambua kwamba umri haufanyi mtu aaminiwe bali matendo yake yanafanya aaminiwe.”​—Rachel.

Biblia inasema: “Endeleeni kuthibitisha jinsi ninyi wenyewe mlivyo.”​—2 Wakorintho 13:5.

  • Jambo la kufikiria: Taja mambo unayoweza kufanya ukitaka wazazi wako wakuamini (au wakuamini tena), na ‘kuthibitisha jinsi ulivyo.’

DOKEZO: Weka malengo, labda kuhusu kudumisha wakati, kumaliza kazi za nyumbani, kurudi nyumbani kwa wakati uliopangiwa, au jambo lingine lolote. Acha wazazi wajue azimio lako na uwaulize wanatarajia ufanye nini ili waweze kukuamini. Kisha fuata kwa bidii himizo hili la Biblia: ‘Vua utu wa zamani unaopatana na mwenendo wako wa zamani.’ (Waefeso 4:​22) Baada ya muda wazazi wako wataona maendeleo yako!

Vijana wenzako wanasema nini

Phoebe

“Usifanye jambo litakalofanya wazazi wako wasikuamini. Wajulishe mambo unayofanya. Wape nafasi ya kutoa mapendekezo kuhusu jinsi unavyoshughulikia mambo. Ikiwa wataona kwamba unafanya maamuzi mazuri, watakuamini zaidi.”​—Phoebe.

Kyle

“Kutumainika hakutokei tu. Ikiwa wazazi wako hawakuamini, kwa kawaida wanakuwa na sababu inayofaa ya kufanya hivyo. Wanapokuamini, hawafanyi hivyo ili watimize matarajio yako. Wanakutumaini kwa sababu wana uhakika utafanya maamuzi ya hekima.”​—Kyle.

Cortlan

“Sikuzote waeleze wazazi wako ukweli, na uwasiliane nao kikamili. Usiwape habari nusu-nusu kiasi kwamba wanahitaji kukuuliza ili wapate habari kamili. Waeleze kila kitu. Watakuamini ikiwa utawaeleza ukweli wote.”​—Cortlan.

Rachel

“Chukua hatua ya kwanza. Fanya kazi zako za nyumbani bila kukumbushwa, na ufanye mengi zaidi ya inavyotarajiwa. Rudi nyumbani mapema kabla ya muda uliopangiwa kurudi. Njia bora ya kutumainiwa ni kuonyesha kwamba unatumainika.”​—Rachel..

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki