Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwyp makala 83
  • Ninaweza Kupinga Vishawishi Jinsi Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ninaweza Kupinga Vishawishi Jinsi Gani?
  • Vijana Huuliza
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Unachopaswa kujua
  • Unachoweza kufanya
  • Jinsi ya Kupinga Vishawishi
    Amkeni!—2014
  • Kushinda Udhaifu wa Kibinadamu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Ninaweza Kupingaje Vishawishi?
    Amkeni!—2008
  • Ninaweza Kupinga Vishawishi Jinsi Gani?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1
Pata Habari Zaidi
Vijana Huuliza
ijwyp makala 83
Kijana akishawishiwa anapoona vijana wawili wakionyeshana mahaba, wavulana wawili wakiangalia kitu kwenye kifaa cha kielektroni, na msichana akipita karibu nao

VIJANA HUULIZA

Ninaweza Kupinga Vishawishi Jinsi Gani?

Mtume Paulo aliandika hivi: “Ninapotaka kufanya yaliyo sawa, yaliyo mabaya yapo pamoja nami.” (Waroma 7:​21) Umewahi kuhisi kama mtume Paulo? Ikiwa ndivyo, makala hii inaweza kukusaidia kupinga kishawishi cha kutenda kulingana na tamaa mbaya.

  • Unachopaswa kujua

  • Unachoweza kufanya

  • Vijana wenzako wanasema nini

Unachopaswa kujua

Ukishinikizwa na vijana wenzako unaweza kushawishiwa kufanya mambo mabaya. Biblia inasema kwamba “watu wabaya hupotosha maadili.” (1 Wakorintho 15:33, maelezo ya chini) Kushinikizwa na watu wengine au vyombo vya habari kunaweza kuchochea tamaa ya moyo wako ambayo inaweza kukushawishi ufanye mambo mabaya na hata kusababisha ‘ufuate umati ili kutenda maovu.’​—Kutoka 23:2.

“Shinikizo la kutaka upendwe na kukubaliwa linaweza kukuongoza ufanye chochote wengine wanachofanya ili tu ukubaliwe nao.”​—Jeremy.

Jambo la kufikiria: Kwa nini inaweza kuwa vigumu kupinga kishawishi ikiwa unajali sana jinsi wengine wanavyofikiri kukuhusu?​—Methali 29:25.

Jambo kuu: Usikubali vijana wenzako wakushinikize upuuze viwango vyako.

Unachoweza kufanya

Elewa mambo unayoamini. Ikiwa hujui mambo unayoamini, unaweza kuwa kama kikaragosi ambacho kinaongozwa na watu wengine. Ni jambo bora zaidi kufuata himizo hili la Biblia: “Hakikisheni mambo yote; shikamaneni na yaliyo mema.” (1 Wathesalonike 5:​21) Kadiri unavyoelewa mambo unayoamini, ndivyo inavyokuwa rahisi zaidi kuishi kulingana na mambo hayo na kupinga kishawishi cha kutenda kinyume na mambo unayoamini.

Jambo la kufikiria: Kwa nini unaamini kwamba viwango vya Mungu vya maadili vimekusudiwa kukunufaisha?

“Nimegundua kwamba wakati wowote ninaposhikamana na kile ninachoamini na kushinda kishawishi, wengine wananiheshimu zaidi.”​—Kimberly.

Mfano wa kuigwa katika Biblia: Danieli. Inawezekana Danieli alikuwa bado tineja “[alipoazimia] moyoni mwake” kwamba angetii sheria za Mungu.​—Danieli 1:8.

Kijana akiwa ameshikwa na kamba, kana kwamba anaongozwa kama kikaragosi

Ikiwa hujui mambo unayoamini, unaweza kuwa kama kikaragosi ambacho kinaongozwa na watu wengine

Tambua udhaifu wako. Biblia inaeleza kuhusu “tamaa za ujana”​—ni tamaa ambazo zinakuwa na nguvu hasa unapokuwa kijana. (2 Timotheo 2:​22) Zinatia ndani si tamaa ya ngono tu, bali pia tamaa ya kukubaliwa na wengine, na tamaa ya uhuru wa kujifanyia maamuzi kabla ya kufikisha umri wa kufanya hivyo.

Jambo la kufikiria: Biblia inasema kwamba “kila mtu hujaribiwa kwa kuvutwa na kushawishiwa na tamaa yake mwenyewe.” (Yakobo 1:​14) Ni tamaa gani iliyo na ushawishi mkubwa kwako?

“Uwe mnyoofu kwa kutambua tamaa zenye ushawishi mkubwa kwako. Fanya utafiti kuhusu jinsi ya kukabiliana na tamaa hizo, na uandike mambo unayoweza kutumia. Kwa njia hiyo, utajua jinsi ya kupinga kishawishi utakapokikabili wakati ujao.”​—Sylvia.

Mfano wa kuigwa katika Biblia: Daudi. Nyakati fulani alifanya maamuzi kwa kushinikizwa na wengine au na tamaa zake mwenyewe. Lakini Daudi alijifunza kutokana na makosa yake na alijaribu kuboresha mambo. Alisali hivi kwa Yehova: “Umba moyo safi ndani yangu . . . na uweke roho mpya ndani yangu, iliyo imara.”​—Zaburi 51:10.

Shinda vishawishi. Biblia inasema hivi: “Usiache ushindwe na uovu.” (Waroma 12:21) Hilo linamaanisha usikubali kishawishi kikushinde. Unaweza kuchagua kufanya jambo linalofaa.

Jambo la kufikiria: Unaweza kuhakikisha jinsi gani kwamba unafanya jambo linalofaa katika hali inayokushawishi ufanye jambo lisilofaa?

“Ninafikiria jinsi nitakavyohisi nikitenda kulingana na jinsi tamaa yangu inavyonishawishi. Je, nitahisi vizuri? Labda, lakini kwa muda mfupi tu. Je, bado nitaendelea kuhisi vizuri hata baada ya muda mrefu kupita? Hapana, badala yake nitahisi vibaya sana. Je, hilo litakuwa na faida? La!”​—Sophia.

Mfano wa kuigwa katika Biblia: Paulo. Ingawa alikubali kwamba alikuwa na mwelekeo mbaya, Paulo aliushinda. Aliandika hivi: “Ninautia nidhamu sana mwili wangu, na kuuongoza kama mtumwa.”​—1 Wakorintho 9:​27, maelezo ya chini.

Jambo kuu: Wewe ndiye unayeamua jinsi ya kukabiliana na kishawishi.

Kumbuka, vishawishi ni vya muda mfupi. Melissa mwenye umri wa miaka 20 anasema hivi: “Mambo mengi ambayo yalikuwa vishawishi vikubwa kwangu wakati nilipokuwa shuleni, sasa si mambo ya muhimu hata kidogo kwangu. Kukumbuka hilo kunanihakikishia kwamba vishawishi vya sasa pia vitapita na siku moja nitatafakari na kutambua kwamba maisha yangu yamekuwa bora kwa sababu nilivipinga.”

Vijana wenzako wanasema nini

Olivia

“Kuweka azimio na kuwa na ujasiri wa kushikamana na azimio langu hunisaidia kupinga kishawishi. Kwa mfano, nikishaamua kutofanya jambo fulani, ninashikamana na uamuzi huo, sifikirii kubadili uamuzi huo au kujiruhusu niongozwe na uamuzi wa mtu mwingine.”​—Olivia.

Jared

“Matineja wanashinikizwa sana kwenda kwenye karamu na kufanya kila kitu kinachofanyika huko​—kunywa pombe, kutumia dawa za kulevya, na kufanya ngono. Nimejionea kwamba kuzungumza waziwazi na wazazi kuhusu mambo hayo kunasaidia sana. Pia, kuwa na jambo la kufanya wakati wa mapumziko kumenisaidia kuepuka kishawishi cha kufanya jambo lisilofaa.”​—Jared.

Mayan

“Mojawapo ya vishawishi vigumu zaidi kukabiliana navyo ni kushawishiwa kufanya jambo fulani ambalo wengine wanaliona kuwa si baya lakini mimi naliona kuwa jambo lisilofaa​—kama vile kuchagua burudani. Unahitaji kuelewa viwango vyako ili kuepuka kushinikizwa kwa njia hiyo na inahitaji wakati na uzoefu ili kufaulu.”​—Mayan.

Julian

“Inapohusu kishawishi, unapaswa kuwa mnyoofu kujihusu. Unapaswa kujua ni maeneo gani katika intaneti ambayo yanaonyesha mambo ya kushawishi, maadili mapotovu, na unapaswa kujua jinsi utakavyotenda mambo hayo yakitokea. Unapaswa kuamua utakavyotenda ili usiingie kwenye kishawishi.”​—Julian.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki