Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 166
  • Je, Pesa Ndio Chanzo cha Uovu Wote?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Pesa Ndio Chanzo cha Uovu Wote?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Biblia inasema nini kuhusu pesa?
  • Kwa nini Biblia inatuonya tusipende pesa?
  • Tunaweza kunufaikaje kutokana na ushauri wa Biblia kuhusu pesa?
  • Pesa
    Amkeni!—2014
  • Maoni Yenye Usawaziko Kuhusu Pesa
    Amkeni!—2015
  • Tunapaswa Kuwa na Maoni Gani Kuhusu Pesa?
    Amkeni!—2007
  • Unaweza Kudumishaje Maoni Yaliyosawazika Kuhusu Pesa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 166
Mtu akijaribu kuchukua kiasi kikubwa cha pesa.

Je, Pesa Ndio Chanzo cha Uovu Wote?

Jibu la Biblia

Hapana. Biblia haisemi kwamba pesa ndio chanzo cha mambo yote mabaya. Watu wengi hutumia usemi “pesa ndio chanzo cha uovu wote,” lakini usemi huo si nukuu kamili la Biblia na unaopotosha. Biblia inasema “kupenda sana fedha ni chanzo cha uovu wote.”a—1 Timotheo 6:10, Biblia Habari Njema.

  • Biblia inasema nini kuhusu pesa?

  • Kwa nini Biblia inatuonya tusipende pesa?

  • Tunaweza kunufaikaje kutokana na ushauri wa Biblia kuhusu pesa?

  • Mistari ya Biblia kuhusu pesa

Biblia inasema nini kuhusu pesa?

Biblia inaonyesha kwamba pesa zinapotumiwa kwa hekima, zinaweza kuwa na faida, hata zinaweza kuwa “ulinzi.” (Mhubiri 7:12) Isitoshe, Biblia inawapongeza wale wanaowaonyesha wengine ukarimu, huenda kwa kuwapa pesa.—Methali 11:25.

Wakati huohuo, Biblia inaonya dhidi ya kutanguliza pesa maishani. Inasema hivi: “Njia yenu ya maisha iwe bila upendo wa pesa, huku mkiridhika na vitu mlivyo navyo.” (Waebrania 13:5) Jambo kuu ni kuwa na usawaziko kuhusu pesa na kutofuatilia utajiri. Badala yake, lengo letu linapaswa kuwa kuridhika na vitu tunavyohitaji hasa, kama vile chakula, mavazi, na makao.—1 Timotheo 6:8.

Kwa nini Biblia inatuonya tusipende pesa?

Watu wenye pupa hawatapata uzima wa milele. (Waefeso 5:5) Sababu moja ni kwamba pupa ni aina fulani ya ibada ya sanamu, au ya uwongo. (Wakolosai 3:5) Sababu nyingine ni kwamba watu wenye pupa wanapojitahidi kupata wanachotamani, mara nyingi wanafanya mambo mabaya. Methali 28:20 inasema kwamba wale ‘wanaoharakisha kupata utajiri hawatabaki bila hatia.’ Huenda hata wakashawishika kujihusisha katika uhalifu, kama vile, kuwatisha wengine, kujihusisha katika unyang’anyi, ulaghai, utekaji-nyara, au uuaji.

Hata ikiwa kupenda pesa hakutaongoza kwenye tabia mbaya, kunaweza kuwa na madhara mengine. Biblia inasema kwamba “wale ambao wameazimia kuwa matajiri huanguka kwenye majaribu, na mtego, na tamaa nyingi za kijinga zenye kudhuru.”—1 Timotheo 6:9.

Tunaweza kunufaikaje kutokana na ushauri wa Biblia kuhusu pesa?

Ikiwa hatutalegeza viwango vya kimaadili na vya kiroho ili tu kupata pesa, tutaendelea kujiheshimu na tutapata kibali na utegemezo wa Mungu. Mungu anawaahidi hivi wale ambao wanajitahidi kumpendeza: “Sitakuacha wala kukutupa kamwe.” (Waebrania 13:5, 6) Pia anatuhakikishia kwamba “mtu mwaminifu atapata baraka nyingi.”—Methali 28:20.

Mistari ya Biblia Kuhusu Pesa

Mhubiri 7:12: ‘Pesa ni ulinzi.’

Maana: Pesa zinapotumiwa kwa hekima zinaweza kuwa na faida kwa sababu zinatoa ulinzi wa kadiri fulani.

Luka 12:15: “Hata mtu anapokuwa na vitu vingi, uhai wake hautokani na vitu alivyo navyo.”

Maana: Pesa si jambo muhimu zaidi maishani, na haziwezi kutusaidia kupata wokovu.

1 Timotheo 6:10: “Kupenda pesa ndicho chanzo cha mambo mabaya ya kila aina, na kwa kujitahidi kufikia upendo huo, wengine wamepotoshwa kutoka kwenye imani na kujichoma kila mahali kwa maumivu mengi.”

Maana: Pesa hazina tatizo. Lakini watu wanaopenda pesa, yaani, wale wanaofanya pesa kuwa jambo kuu maishani mwao, wanajisababishia matatizo, kama vile kuvunjika kwa familia na matatizo ya afya kwa sababu ya kufanya kazi kupita kiasi.

Waebrania 13:5: “Njia yenu ya maisha iwe bila upendo wa pesa, huku mkiridhika na vitu mlivyo navyo.”

Maana: Badala ya kufuatilia pesa kupita kiasi, ni jambo la hekima kuridhika na mambo tunayohitaji kabisa.

Mathayo 19:24: “Ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”

Maana: Yesu alikuwa amemwalika mwanamume fulani kijana aliyekuwa tajiri amfuate. Mwanamume huyo alikataa kwa sababu alipenda sana mali zake. Kwa hiyo, Yesu alitoa onyo. Mtu anayetanguliza utajiri badala ya kumtanguliza Mungu anaweza kukosa uzima wa milele.

a Mstari huo umetafsiriwa pia kuwa: “Kupenda pesa ndicho chanzo cha mambo mabaya ya kila aina.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki