11 Yuda akamwambia Tamari binti mkwe wake: “Ishi ukiwa mjane katika nyumba ya baba yako mpaka Shela mwanangu atakapokua,” kwa maana Yuda alisema moyoni mwake: ‘Huenda yeye pia akafa kama ndugu zake.’+ Basi Tamari akaenda kuishi katika nyumba ya baba yake.