14 Ndipo akayavua mavazi yake ya ujane, akajifunika uso kwa shela na kujifunika mabegani kwa mtandio, akaketi chini kwenye lango la kuingia Enaimu, jiji lililo katika barabara inayokwenda Timna, kwa sababu aliona kwamba Shela amekuwa mtu mzima lakini hajaruhusiwa amwoe.+