19 Akasema: “Ni jambo nisiloweza kamwe kuwazia, kulingana na maoni ya Mungu wangu, kufanya hivyo! Je, ninywe damu ya wanaume hawa waliohatarisha uhai wao?”+ Kwa maana walihatarisha uhai wao kwenda kuyaleta. Basi akakataa kuyanywa. Hayo ndiyo mambo waliyotenda mashujaa wake watatu hodari.