28 Naye amenitendea kwa upendo mshikamanifu mbele ya mfalme,+ washauri wake,+ na wakuu wote wa mfalme wenye nguvu. Hivyo nikajipa ujasiri kwa sababu mkono wa Yehova Mungu ulikuwa juu yangu, nami nikawakusanya wanaume waliokuwa viongozi katika Israeli ili wapande pamoja nami.