-
Marko 16:20Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo
-
-
20 Basi, wao wakatoka kwenda na kuhubiri kila mahali, huku Bwana akifanya kazi pamoja nao na kutegemeza huo ujumbe kupitia ishara zenye kuandamana.
UMALIZIO MFUPI
Hati na tafsiri fulani za mwisho-mwisho zina umalizio mfupi baada ya Marko 16:8, kama ifuatavyo:
Lakini mambo yale yote yaliyokuwa yameamriwa wakayasimulia kwa ufupi kwa wale waliomzunguka Petro. Zaidi, baada ya mambo hayo, Yesu mwenyewe akapeleka kupitia wao kutoka mashariki hadi magharibi mbiu iliyo takatifu na isiyofisidika ya wokovu udumuo milele.
-