34 “Naye kuhani atatazama kule kuanguka kwa nywele kusiko kwa kawaida katika siku ya saba; na ikiwa kule kuanguka kwa nywele kusiko kwa kawaida hakujaenea katika ngozi, wala haionekani kwamba kumepenya chini ya ngozi, ndipo kuhani atamtangaza kuwa safi,+ naye atayafua mavazi yake na kuwa safi.