Maelezo ya Ziada
^ [1] (fungu la 14) Utekwa wa Wayahudi wa miaka 70 huko Babiloni una ulinganifu mkubwa na kilichowapata Wakristo baada ya uasi imani kutokea. Hata hivyo, haielekei kwamba utekwa wa Kiyahudi ni mfano wa kinabii wa mambo yaliyowapata Wakristo. Jambo moja linalofanya tufikie mkataa huo ni kwamba kipindi cha utekwa kinatofautiana. Kwa hiyo, hatupaswi kulinganisha mambo hususa yaliyowapata Wayahudi walipokuwa utekwani na hali iliyowapata Wakristo watiwa mafuta katika miaka iliyotangulia mwaka 1919.