Maelezo ya Chini
b Unajisi katika ndoa hutukia wakati mume anapomshinda nguvu mke wake na kufanya ngono kwa nguvu. Huenda waume wengine wakaamini kwamba “mamlaka” ambayo mtume Paulo anasema mwanamume anayo juu ya mwili wa mke wake ni kamili. Hata hivyo, Paulo pia alisema kwamba ‘waume wapaswa kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe.’ Mtume Petro asema kwamba waume wapaswa ‘kuwapa wake zao heshima, kama chombo kisicho na nguvu.’ Hiyo inapinga jeuri au ngono ya kulazimishwa.—1 Wakorintho 7:3-5; Waefeso 5:25, 28, 29; 1 Petro 3:7; Wakolosai 3:5, 6; 1 Wathesalonike 4:3-7.