Maelezo ya Chini
a Wakiwa na hamu ya kuja kwa pili kwa Yesu, Mashahidi wa Yehova wamedokeza tarehe zilizogeuka kuwa zenye kosa. Kwa sababu hiyo, wengine wamewaita manabii bandia. Hata hivyo, katika pindi hizo, hawakudhubutu kutoa utabiri mbalimbali ‘katika jina la Yehova.’ Hawakusema kamwe, ‘Haya ni maneno ya Yehova.’ Mnara wa Mlinzi, jarida rasmi la Mashahidi wa Yehova, limesema: “Sisi hatuna kipawa cha kutoa unabii.” (Januari 1883, ukurasa 425 Kiingereza) “Wala maandishi yetu hayapaswi kuabudiwa wala kuonwa kuwa yasiyokosea.” (Desemba 15, 1896, ukurasa 306) Mnara wa Mlinzi limesema pia kwamba uhakika wa kwamba wengine wana roho ya Yehova “haumaanishi wale wanaotumikia wakiwa Mashahidi wa Yehova wamepuliziwa. Haumaanishi kwamba maandishi katika gazeti hili Mnara wa Mlinzi yamepuliziwa na hayawezi kukosea na hayana makosa.” (Mei 15, 1947, ukurasa 157) “Mnara wa Mlinzi halidai kuwa limepuliziwa kwa yale linayosema, wala si lisiloweza kupingwa.” (Agosti 15, 1950, ukurasa 263) “Akina ndugu wanaotayarisha vichapo hivyo wanakosea. Maandishi yao hayajapuliziwa kama yale ya Paulo na waandikaji wengine wa Biblia. (2 Tim. 3:16) Na hivyo, nyakati nyingine imekuwa lazima kusahihisha maoni, kadiri uelewevu ulivyoongezeka. (Mit. 4:18)”—Februari 15, 1981, ukurasa 19.