Maelezo ya Chini
a Kutenda watoto vibaya kingono hutukia wakati mtu anapomtumia mtoto ili kutosheleza tamaa zake za kingono. Mara nyingi kunatia ndani kile ambacho Biblia huita uasherati, au por·neiʹa, ambayo yaweza kutia ndani kupapasa-papasa viungo vya uzazi, kufanya ngono, na ngono ya kutumia mdomo au ya mkundu. Matendo fulani mabaya, kama vile kupapasa-papasa matiti, matongozi mabaya yasiyo ya adili, kumwonyesha mtoto pornografia, kumtazama akiwa uchi, na kumfunua mavazi isivyofaa, yaweza kujumlika kuwa yale Biblia inayoshutumu kuwa “mwenendo mlegevu.”—Wagalatia 5:19-21, NW; ona Mnara wa Mlinzi la Januari 1, 1984, kielezi chini ukurasa 6.