Maelezo ya Chini
b Wakristo wa karne ya kwanza ambao Paulo aliwaandikia walikuwa na tumaini la ufufuo wa kwenda mbinguni ambako wangetumikia wakiwa watawala-wenzi pamoja na Kristo. (1 Wathesalonike 4:14-17; linganisha Luka 22:29, 30.) Hivyo Paulo aliwatia moyo wafarijiane kwa tumaini la kwamba kwenye kuwapo kwa Kristo waaminifu miongoni mwao waliokuwa wamekufa wangefufuliwa na wangeunganishwa pamoja na Kristo na pamoja na mtu na mwenzake. Hata hivyo, kwa walio wengi sana kati ya wale waliokufa, Biblia hutoa tumaini la ufufuo wa kuingia katika paradiso ya kidunia iliyorudishwa.—Yohana 5:28, 29; Ufunuo 21:1-4.