Maelezo ya Chini
a Katika 1844, kasisi Mwingereza, E. B. Elliott, alitoa uangalifu kwa 1914 kuwa wakati huenda zile “nyakati saba” za Danieli sura ya 4 zingeisha. Katika 1849, Robert Seeley, wa London, alishughulika na habari hiyo kwa njia hiyohiyo. Joseph Seiss, wa Marekani, alielekeza kwenye 1914 kuwa tarehe muhimu katika kronolojia ya Biblia katika kichapo kilichohaririwa karibu na 1870. Katika 1875, Nelson H. Barbour aliandika katika gazeti lake Herald of the Morning kwamba 1914 iliweka alama mwisho wa kipindi kile Yesu alichokiita “nyakati zilizowekwa za mataifa.”—Luka 21:24, NW.