Maelezo ya Chini
b Mashimo meusi yafahamika kuwa vizio vya anga ambavyo katika hivyo nyota ama nyota mbalimbali zimeporomokea na “ambapo kani za kiuvutano huwa na nguvu sana hivi kwamba huzuia kuponyoka kwa hata chembe zilizo mwendoni wa kasimwelekeo ya nuru [kilometa 300,000 kwa sekunde].” Hivyo, “hakuna nuru, dutu ama ishara ya aina yoyote iwezayo kuponyoka.”—The International Encyclopedia of Astronomy.