Maelezo ya Chini
b Toleo la Mnara wa Mlinzi la Septemba 1, 1997, ukurasa wa 21-22, lilitaarifu: “Mashahidi wa Yehova wamekuwa na hamu ya kujua wakati ambapo siku ya Yehova itatukia. Nyakati nyingine kwa sababu ya hamu yao wamejaribu kukadiria wakati ambao huenda siku hiyo ikaja. Lakini kwa kufanya hivyo, kama vile walivyofanya wanafunzi wa mapema wa Yesu, wameshindwa kutii onyo la Bwana-Mkubwa wao kwamba “sisi ha[tu]jui ni lini ulio wakati uliowekwa rasmi.” (Marko 13:32, 33) Wadhihaki wamewadhihaki Wakristo waaminifu kwa sababu ya mataraja yao ya kabla ya wakati. (2 Petro 3:3, 4) Hata hivyo, Petro athibitisha kwamba siku ya Yehova itakuja, kulingana na ratiba Yake.”