Maelezo ya Chini
a AD ilipata jina kutokana na Alois Alzheimer, ambaye alikuwa tabibu wa Ujerumani aliyeyafafanua maradhi hayo kwa mara ya kwanza katika 1906 baada ya kuchunguza maiti ya mtu aliyekuwa na kasoro kubwa ya akili. Inafikiriwa kwamba AD hufanyiza karibu asilimia 60 ya visa vyote vya kasoro za akili, ikiathiri kufikia sehemu moja kwa kumi ya watu wenye umri uzidio miaka 65. Kasoro nyingine ya akili, multi-infarct dementia, husababishwa na mishtuko kidogo-kidogo ya akili, ambayo hudhuru ubongo.