Maelezo ya Chini
b Tahadhari: Ni lazima mtu achunguzwe kabisa kitiba kabla ya kuamuliwa kuwa ana AD. Asilimia 10 hadi 20 hivi ya visa vya kasoro za akili hutokana na magonjwa ambayo yanaweza kutibiwa. Kwa habari ya kutambua AD, kitabu How to Care for Aging Parents chaeleza: “Alzheimer yaweza kutambuliwa kwa uhakika kabisa kwa kuchunguza ubongo wakati wa kuchunguza maiti, lakini madaktari waweza kuondoa uwezekano wa magonjwa mengine kwa kuchunguza dalili zake.”