Maelezo ya Chini
a Toleo la Mnara wa Mlinzi la Oktoba 15, 1991, ukurasa wa 31, huandaa mwelekezo ufuatao: “Mkristo wa kweli apaswa afikirie hili: Je! kufuata desturi fulani kungeonyesha wengine kwamba nimechagua imani au mazoea yasiyo ya Kimaandiko? Kipindi cha wakati na mahali vingeweza kuongoza jibu la hilo. Desturi (au pambo) huenda ikawa ilikuwa na maana ya kidini bandia mamileani yaliyopita au huenda ikawa na maana hiyo leo katika nchi ya mbali. Lakini bila kuchukua wakati mwingi katika kuchunguza hilo, jiulize mwenyewe hivi: ‘Maoni ya kawaida mahali ninapoishi ni gani?’—Linganisha 1 Wakorintho 10:25-29.”