Maelezo ya Chini
b Mojawapo ya vimeng’enya ambavyo watu wengi hukosa mwilini ni laktasi. Wanaokosa kimeng’enya hicho hawawezi kulishiza laktosi katika maziwa, nao huwa wagonjwa wanapokunywa maziwa. Watu wengine wana upungufu wa kimeng’enya kinachomeng’enya tyramine mwilini, kemikali inayopatikana katika jibini na katika vyakula vinginevyo. Wanapokula vyakula vya aina hiyo, wanapatwa na ugonjwa wa kipandauso.