Maelezo ya Chini
a Mashahidi wa Yehova huiona kazi yao ya kuhubiri kuwa ya lazima kwa Wakristo wa kweli—kama alivyofanya mtume Paulo. Yeye alisema hivi: “Ikiwa, sasa, ninatangaza habari njema, hiyo si sababu ya mimi kujisifu, kwa maana nimewekewa sharti.” (1 Wakorintho 9:16) Hata hivyo, kazi yao ya kuhubiri ni kazi ya kujitolea kwa sababu wamechagua kwa hiari kuwa wanafunzi wa Kristo, wakijua kabisa madaraka yanayoambatana na pendeleo hilo.