Maelezo ya Chini
c Vasili Mkalavishvili alifukuzwa kutoka Kanisa Othodoksi la Georgia katikati ya miaka ya 1990 baada ya kuchambua vikali kanisa hilo kwa sababu lilijiunga na Baraza la Makanisa Ulimwenguni. (Kwa sasa Kanisa Othodoksi la Georgia limejitenga na Baraza hilo.) Sasa, Mkalavishvili amejiunga na dini ya Calendarist wa Kale wa Ugiriki inayoongozwa na Askofu Mkuu Cyprian.