Maelezo ya Chini
e Baadhi ya wagonjwa hao walisaidiwa na dawa za kumeza. Dawa hizo zatia ndani zile ambazo huchochea kongosho kutokeza insulini zaidi, nyingine hudhibiti ongezeko la sukari katika damu, na nyingine huwezesha chembe za mwili kupokea insulini. (Kwa kawaida, watu wanaougua ugonjwa wa kisukari wa Aina ya 1 hawapewi dawa za kumeza.) Kwa sasa, insulini haiwezi kumezwa kama dawa za kawaida, kwani protini hiyo humeng’enywa kabla haijafika kwenye damu. Hata ikiwa mgonjwa anatumia insulini na dawa za kumeza, bado anahitaji kufanya mazoezi na kupata lishe bora.