Maelezo ya Chini
a Kulingana na kitabu Modern Blood Banking and Transfusion Practices, cha Dakt. Denise M. Harmening, “madhara yanayosababishwa na kuharibika kwa chembe nyekundu za damu” yanaweza kumpata “mgonjwa ambaye hapo awali aliathiriwa na utiaji wa damu, mimba, au kupachikwa kiungo cha mwili.” Katika hali kama hizo, kinga za mwili zinazosababisha mgonjwa aathiriwe anapotiwa damu mishipani, “hazitambuliwi na uchunguzi unaofanywa kabla ya kutiwa damu.” Kulingana na kitabu Dailey’s Notes on Blood, kuharibika kwa chembe nyekundu za damu “kwaweza kuanza hata wakati kiasi kidogo tu cha damu isiyofaa . . . kinapotiwa mishipani. Njia ya mkojo inapofunga kabisa, mgonjwa hutiwa sumu hatua kwa hatua kwa sababu figo haziwezi kuondoa uchafu kutoka katika damu.”